Siku ya Sabato ilipokwisha kupita, kesho yake siku ya kwanza ya juma, kwa wakati wa mapambazuko, Maria wa Magdala na Maria mwingine wakaenda kuangalia kaburi.
Asubui mapema Yoshua pamoja na watu wote wa Israeli walianza safari kutoka Sitimu. Walipofika kwa muto Yordani, walipiga kambi hapo kwa muda mbele ya kuvuka.
Ilipofika mara ya saba, wakati makuhani walipokwisha kupiga mabaragumu, Yoshua akawaambia watu: “Mupige kelele, kwa kuwa Yawe amekwisha kuwapa huu muji!
Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.