14 Kwa siku ya pili, waliuzunguka ule muji mara moja; na kurudi tena katika kambi kwao. Wakafanya hivyo kwa muda wa siku sita.
Basi, Yoshua akawaamuru wale watu wauzunguke muji mara moja kila siku wakiwa wanabeba Sanduku la Agano la Yawe na kurudi katika kambi kulala usiku.
Wale makuhani saba wenye mabaragumu saba ya kondoo dume walitembea mbele ya Sanduku la Yawe wakipiga mabaragumu kwa mufululizo. Watu wenye silaha walilitangulia Sanduku la Yawe na walinzi wengine nyuma yake. Mabaragumu yakaendelea kupigwa.
Siku ya saba, waliamuka asubui mapema, wakauzunguka muji ule mara saba. Ilikuwa ni siku hiyo tu ambayo waliuzunguka muji ule mara saba.
Wewe na wale watu wenye silaha wote mutauzunguka ule muji mara moja kila siku kwa muda wa siku sita.