Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwa hiyo ilikuwa watoto wa watu hao ambao Yawe aliowakomalisha kwa pahali pao. Na ni hao ndio Yoshua aliowatahiri, maana hawakukuwa wanatahiriwa wakati ule walipokuwa katika safari ndani ya jangwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 5:7
5 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakawaambia: “Hatuwezi kumwoesha dada yetu kwa mutu asiyetahiriwa. Kufanya hivyo ni haya kwetu.


Ninyi mulisema kwamba watoto wenu watakamatwa mateka, lakini mimi nitawafikisha watoto wenu katika inchi muliyoizarau, kusudi waijue na ikuwe makao yao.


Kisha Yawe akatuambia sisi wote: ‘Hao watoto wenu munaoogopa kwamba watakuwa mateka za waadui zenu, hakika hao wanaokuwa wadogo ambao hawajui bado kupambanua kati ya mazuri na mabaya, hao ndio watakaoingia huko, nami nitawapa wao inchi hiyo ikuwe yao.


Waisraeli walisafiri kwa muda wa miaka makumi ine katika jangwa hata wanaume wote waliokuwa na umri wa kwenda kwa vita wakaangamia kwa kuwa hawakusikiliza mambo Yawe aliyosema. Yawe alikuwa amewaapia watu hao kwamba hawataiona inchi ile inayotiririka maziwa na asali ambayo yeye aliwaapia baba zao kwamba atawapa.


Wanaume wote walipokwisha kutahiriwa walikaa katika kambi mpaka walipopona.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ