Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 5:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Waisraeli walisafiri kwa muda wa miaka makumi ine katika jangwa hata wanaume wote waliokuwa na umri wa kwenda kwa vita wakaangamia kwa kuwa hawakusikiliza mambo Yawe aliyosema. Yawe alikuwa amewaapia watu hao kwamba hawataiona inchi ile inayotiririka maziwa na asali ambayo yeye aliwaapia baba zao kwamba atawapa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 5:6
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wamoja walitangatanga katika jangwa tupu, hawakuweza kufikia katika muji wa kukaa.


Ninaahidi kwamba nitawatoa katika mateso yenu kule Misri na kuwapeleka katika inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. Nitawapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali.’


na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.


Hata hivyo, niliwaapia kulekule katika jangwa kwamba sitawaingiza katika inchi niliyowapa, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote.


Siku hiyo niliwaapia kwamba nitawatoa katika inchi ya Misri na kuwapeleka mpaka kwenye inchi niliyowachagulia, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote.


atakayeona inchi ile niliyoapa kuwapatia babu zao. Vilevile hata wale wanaonizarau hawataiona.


Hao ndio wanaume Waisraeli waliohesabiwa na Musa na kuhani Eleazari katika inchi za mabonde za Moabu, ngambo ya muto Yordani, karibu na Yeriko.


Siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, mwaka wa makumi ine nyuma ya kutoka Misri, Musa akawaambia watu kila kitu ambacho Yawe alimwamuru awaambie.


Miaka makumi tatu na nane ilikuwa imepita tangu kuondoka Kadesi-Barnea mpaka kuvuka kijito Zeredi. Wakati huo, wote wenye umri wa kwenda kwa vita waliotoka Misri walikuwa wamekwisha kufa, kulingana na jinsi Yawe alivyowaapia.


“Basi, mukumbuke jinsi Yawe Mungu wenu alivyowabariki ninyi katika kila jambo mulilofanya. Aliwatunza mulipokuwa munatangatanga katika jangwa hili kubwa. Amekuwa pamoja nanyi miaka hii yote makumi ine na hamukupungukiwa na kitu chochote.


Wakati huo wa miaka makumi ine nguo zenu hazikuchakaa, wala miguu yenu haikuvimba.


Basi nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia kwenye mapumziko niliyowatayarishia!”


Ukuwe imara na hodari kwa sababu wewe utawaongoza watu hawa kuirizi inchi ambayo niliwaahidi kwamba nitawapa wazee wao.


Waisraeli waliponililia mimi Yawe, niliweka giza kati yao na Wamisri na kuifanya bahari iwafunike Wamisri. Ninyi wenyewe mulijionea yale niliyowatendea Wamisri. Muliishi katika jangwa muda murefu.


Hao wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini wale wote waliozaliwa katika safari kule katika jangwa kisha kutoka Misri, walikuwa bado hawajatahiriwa.


Kwa hiyo ilikuwa watoto wa watu hao ambao Yawe aliowakomalisha kwa pahali pao. Na ni hao ndio Yoshua aliowatahiri, maana hawakukuwa wanatahiriwa wakati ule walipokuwa katika safari ndani ya jangwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ