Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 5:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Naye akamujibu: “Wala wenu wala wa waadui zenu! Lakini mimi ni jemadari wa jeshi la Yawe, na sasa nimefika.” Yoshua akainama chini kwa heshima, kisha akamwuliza: “Bwana wangu, unataka mimi mutumishi wako nifanye nini?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 5:14
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hapo Abrahamu akainama uso mpaka chini, akacheka ndani ya moyo wake akiwaza: “Itawezekana kweli mutoto kuzaliwa kwa muzee wa miaka mia moja? Na namna gani, Sara ambaye umri wake ni miaka makumi tisa, ataweza kupata mutoto?”


Abramu akaanguka uso mpaka chini. Naye Mungu akamwambia:


Tena jambo hili lilikuwa dogo mbele ya macho yako. Zaidi ya hayo, Bwana wangu Yawe, umeahidi kuchunga jamaa yangu kwa miaka mingi inayokuja na kunijulisha hivyo, ee Bwana wangu Yawe.


Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi? Maana wewe unanijua mimi mutumishi wako, ee Bwana wangu Yawe!


Zaburi ya Daudi. Yawe anamwambia bwana wangu: “Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu mpaka nitakapowaweka waadui zako chini ya miguu yako.”


Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu? Ni Yawe, wa majeshi, yeye ndiye Mufalme mwenye utukufu.


Lakini Musa akamwambia Yawe: “Ewe Bwana wangu, mimi mutumishi wako sina ufundi wa kusema tangu zamani, hata kisha kusema nawe. Ulimi wangu ni muzito.”


Lakini Musa akasema: “Ee Bwana wangu, tafazali ninakusihi, umutume mutu mwingine.”


Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.


Kisha nikamusikia Yawe akisema: Nimutume nani? Ni nani atakayekuwa mujumbe wetu? Nami nikajibu: Niko hapa! Unitume mimi.


Basi, nikasimama na kwenda katika bonde. Nikiwa huko nikauona utukufu wa Yawe ukiwa umesimama huko kama utukufu ule niliokuwa nimeuona karibu na muto Kebari; nami nikaanguka uso mpaka chini.


Mukubwa wa ufalme wa Persia alinipinga kwa muda wa siku makumi mbili na moja. Lakini Mikaeli, mumoja kati ya wakubwa, akakuja kunisaidia, kwa hiyo nikamwacha kule pamoja na mukubwa wa ufalme wa Persia,


Lakini nitakujulisha yale yaliyoandikwa katika kitabu cha ukweli. Sina mwingine wa kunisaidia kwa kuwashinda hawa isipokuwa Mikaeli, malaika mulinzi wenu.


Wakati huo, Mikaeli, malaika mukubwa, anayekuwa mulinzi wa watu wako, atatokea. Halafu kutakuwa wakati wa taabu sana kuliko nyakati zingine zote tangu mataifa yalipoanza kuwa katika dunia. Lakini, wakati huo, kila mumoja wa watu wako ambaye jina lake limeandikwa katika kitabu cha uzima, ataokolewa.


Pembe dogo ile ikajitukuza mbele ya mukubwa wa viumbe vya mbinguni. Ikakomesha sadaka za kuteketezwa kwa moto ambazo mukubwa wa viumbe vya mbinguni alivyotambikiwa kila siku, na kuchafua hekalu lake.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Hapo, Yawe akafungua macho ya Balamu, naye akamwona malaika wa Yawe amesimama katika njia, akishika upanga uliochomolewa toka kifuko chake. Balamu akajitupa uso mpaka chini.


‘Bwana wetu Mungu alimwambia Bwana wangu: Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu mpaka nitakapoweka waadui zako chini ya miguu yako.’


Halafu mutu mumoja mwenye ukoma akakuja, akapiga magoti mbele yake na kumwambia: “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”


Namna gani nimepata bahati hii ya kutembelewa na mama ya Bwana wangu?


Daudi yeye mwenyewe alisema katika kitabu cha Zaburi: ‘Bwana wetu Mungu alimwambia Bwana wangu: Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu


Yesu alipokuwa katika muji mumoja kati ya miji ile, kukatokea mutu aliyejaa na ukoma mwili wote. Naye alipomwona Yesu, akainama uso mpaka chini, akamusihi akisema: “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


Lakini simama, uingie katika muji, na mule watakuambia jambo unalopaswa kufanya.”


Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo


Kwa hiyo ilifaa kwamba Mungu aliyeumba vitu vyote na kuvilinda imara, amufanye Yesu kuwa mukamilifu kwa njia ya mateso, kusudi awalete watoto wengi kuwa washiriki wa utukufu wa Mungu. Kwa maana Yesu ndiye anayewaongoza watu wapate kuokoka.


Halafu kukatokea vita katika mbingu. Mikaeli na wamalaika zake wakapigana na yule nyoka mukubwa. Naye yule nyoka akapigana nao pamoja na wamalaika zake,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ