Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Siku moja Yoshua alipokuwa karibu na muji wa Yeriko, aliona kwa rafla mutu mumoja akisimama mbele yake na upanga uliochomolewa katika mukono wake. Yoshua akamwendea, akamwuliza: “Wewe ni wetu au ni wa waadui zetu?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 5:13
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alimutokea Abrahamu kwenye miti ya mielo ya Mamure. Abrahamu alikuwa anaikaa kwenye mulango wa hema yake wakati wa joto la muchana.


Alipoinua macho yake, akaona watu watatu wakisimama mbali kidogo mbele yake. Mara tu alipowaona, akakimbia kutoka kwenye mulango wa hema yake, akakwenda kuwapokea. Alipowafikia akainama kwa heshima


Kisha Yakobo akaamuka toka usingizi, akasema: “Hakika, Yawe yuko pahali hapa, nami sikujua!”


Basi, Yakobo akainua macho, akamwona Esau akikuja pamoja na watu mia ine. Halafu, akawagawanya watoto wake kati ya Lea, Rakeli na wale wajakazi wawili.


Esau alipoinua macho na kuwaona wale wamama na watoto, akauliza: “Ni wa nani hawa unaokuwa nao?” Yakobo akamujibu: “Hawa ni watoto ambao Mungu, kwa neema yake, amenijalia mimi mutumishi wako.”


Wakamusaidia Daudi kupigana na makundi ya washambulizi, maana wote walikuwa waaskari mashujaa na majemadari wa waaskari.


Halafu, Yawe akamwamuru malaika, naye akaweka upanga wake ndani ya mufuko wake.


Lakini Daudi hakuweza kwenda kule kumwomba Mungu shauri kwa sababu alikuwa anaogopa upanga wa malaika wa Yawe.


Malaika wangu atakapowaongoza na kuwafikisha katika inchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanana, Wahivi na Wayebusi, nami nitawaangamiza wale wote.


Nikainua macho, nikamwona mutu anayevaa nguo za kitani naye alikuwa amejifunga mukaba wa zahabu safi kutoka Ufasi.


Nilipoinua macho yangu, niliona kondoo dume amesimama kando ya muto huo. Kondoo huyo alikuwa na pembe mbili ndefu, lakini moja ilikuwa ndefu zaidi, nayo ilitokea nyuma ya ile ingine.


Wakati wa usiku, nilimwona malaika akipanda juu ya farasi mwekundu. Malaika yule alikuwa akisimama katika bonde, katikati ya miti ya mihadasi. Nyuma yake kulikuwa farasi wengine wekundu, wa kijivujivu na weupe.


Basi, punda akamwona malaika huyo wa Yawe amesimama katika njia, akishika upanga uliochomolewa. Kwa hiyo akaacha njia, akaenda pembeni. Balamu akamupiga huyo punda, akamurudisha katika njia.


Hapo, Yawe akafungua macho ya Balamu, naye akamwona malaika wa Yawe amesimama katika njia, akishika upanga uliochomolewa toka kifuko chake. Balamu akajitupa uso mpaka chini.


Walipokuwa wangali wakiangalia mbinguni wakati Yesu alipopanda, kwa rafla kukaonekana watu wawili wanaovaa nguo nyeupe, wakasimama karibu nao.


Yawe akamwambia Yoshua: “Mimi nitautia katika mikono yako muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake na waaskari wake shujaa.


Na katikati ya vile vinara saba, nikaona kiumbe kimoja kinachofanana na Mwana wa Mutu. Naye alikuwa amevaa kanzu ndefu inayofika hata kwenye miguu yake na mukaba wa zahabu katika kifua chake.


Manoa akafuatana naye mpaka kwa mutu huyo, akamwuliza: “Wewe ni yule mutu aliyezungumuza na mwanamuke huyu?” Yule mutu akamujibu: “Ni mimi.”


Basi, Manoa akamwambia muke wake: “Hakika tutakufa, maana tumemwona Mungu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ