11 Kesho yake, ni kusema nyuma ya Pasaka, walikula mikate isiyotiwa chachu na mbegu zenye kukaangwa kutokana na mazao ya inchi ile.
Mbele ya siku hiyo ya kuniletea mimi Mungu wenu sadaka hiyo, hamuruhusiwi kula mazao ya kwanza ya mavuno yenu, yakuwe mabichi, yamekaangwa au yemepikwa kuwa mikate. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu pahali popote mutakapoishi.
Siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo, sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu itaanza. Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu.
kila mara mutakapokula mazao ya inchi hiyo, mutatenga sehemu fulani na kunipa mimi Yawe.
Waisraeli walipokuwa wamepiga kambi kule Gilgali wakafanya sikukuu ya Pasaka magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi katika mabonde ya Yeriko.
Basi, tangu siku hiyo walipokula mazao ya inchi hiyo, Waisraeli hawakupata mana tena. Tangu mwaka ule Waisraeli walikula mazao ya inchi ya Kanana.