Na hivi ndivyo mutakavyokula nyama yule: mutakuwa tayari kwa kusafiri, na kuvaa viatu na kuwa na fimbo zenu katika mikono. Tena mutamukula kwa haraka. Hiyo ni Pasaka ya Yawe.
Basi, mutakula mikate isiyotiwa chachu kuanzia magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, mpaka magaribi ya siku ya makumi mbili na moja ya mwezi uleule wa kwanza.
Lakini kundi la waaskari la Wakaldea liliwafuatilia na kumukamata Zedekia karibu na Yeriko. Kisha kumukamata walimufikisha kwa Nebukadneza, mufalme wa Babeli huko Ribla, katika inchi ya Hamati, naye akamuhukumu.
Wao ni watu waasi. Basi, ewe mwanadamu, ufanye kama vile unakwenda katika uhamisho: ondoka muchana wakati wanapokuwa wakikuona, ukimbilie pahali pengine. Kwenda na muzigo wako kama mukimbizi kutoka pahali unapokuwa mpaka pahali pengine wao wakikuona. Labda wataelewa, ingawa wao ni waasi.
Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!
Basi, wakamwendea Yoshua katika kambi kule Gilgali, wakamwambia yeye na Waisraeli: “Sisi tumetoka katika inchi ya mbali. Tafazali tunaomba mufanye agano nasi.”