Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 4:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 kusudi watu wote wa dunia wajue kwamba mukono wa Yawe una nguvu; nanyi mupate kumwogopa Yawe, Mungu wenu, milele.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 4:24
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

kusudi wakutii wakati wote wanapoishi katika inchi uliyowapa babu zetu.


Nayo mataifa yote katika ulimwengu yatajua kwamba kweli Yawe ndiye Mungu wala hakuna mwingine.


Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe tu, ee Yawe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”


Halafu akarudi kwa mutu wa Mungu pamoja na watu wake, akasema: “Sasa ninajua kwamba hakuna Mungu yeyote katika dunia lakini tu Mungu wa Israeli; kwa hiyo, tafazali sasa upokee zawadi ya mutumishi wako.”


Utajiri na heshima vinatoka kwako, vyote unavitawala. Uwezo na nguvu viko katika mukono wako, nawe unawatukuza wale unaowapenda, na kuwaimarisha wote.


Una nguvu kama mimi Mungu? Unaweza kunguruma kwa sauti kama yangu?


Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi, kusudi aonyeshe nguvu yake kubwa.


Wewe uliumba kaskazini na kusini; milima Tabori na Hermoni inakushangilia.


Nani katika mbingu anayeweza kulinganishwa nawe, ee Yawe? Nani anayekuwa sawa nawe kati ya miungu?


Waisraeli walipoona tendo hilo la ajabu Yawe alilofanya mbele ya Wamisri, wakamwogopa. Wakamwamini Yawe na Musa mutumishi wake.


Kitisho na hofu vimewashika. Kwa sababu ya ukubwa wa nguvu zako, wao wamenyamaza kimya kama jiwe, mpaka watu wako, ee Yawe, wapite, mpaka watu wale uliowakomboa wamewapita.


Musa akawaambia: Musiogope, maana Mungu amekuja kuwapima kusudi mupate kumwogopa siku zote na musitende zambi.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Nitafanya nao agano la milele, kwamba sitaacha kuwatendea mema hata kidogo; nitaweka ndani ya mioyo yao utii kwa ajili yangu kusudi wasiniache tena.


Mataifa yote katika dunia yakiona kwamba ninyi munaitwa kwa jina la Yawe yatawaogopa.


Wakati wote munapokuwa wazima, mutapaswa kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kutii masharti yote na amri ninazowapa ninyi na wazao wenu kusudi mupate kuishi maisha marefu.


Siku ya leo, Yawe atakutia katika mikono yangu. Nitakushinda, nitakukata kichwa chako; na miili ya waaskari wa Wafilistini nitawapa ndege na nyama wa pori. Halafu dunia nzima itajua kwamba Mungu yuko katika Israeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ