21 Kisha Yoshua akawaambia Waisraeli: “Watoto wenu watakapowauliza kwa siku zinazokuja: ‘Mawe haya yana maana gani?’
Kama kisha mwana wako akiuliza maana ya jambo hili, utamwambia: ‘Kwa nguvu ya mukono wake, Yawe alitutoa katika inchi ya Misri ambako tulikuwa watumwa.
Yoshua akayasimika yale mawe kumi na mawili ambayo waliyatwaa kutoka muto Yordani, kule Gilgali.
Mutawaambia hivi: ‘Taifa la Israeli lilivuka muto huu wa Yordani pahali pakavu.’
Jambo hilo litakuwa kitambulisho kati yenu; na watoto wenu watakapowauliza kwa siku zinazokuja: ‘Mawe haya yana maana gani kwenu?’