uwaagize hivi: ‘Mutwae mawe kumi na mawili kutoka hapa katikati ya muto Yordani, kutoka hapa miguu ya makuhani ilipokuwa, mutwae mawe hayo, muyaweke pahali pale ambapo mutalala leo hii.’ ”
Wale wanaume wakafanya kama vile walivyoamriwa na Yoshua, wakatwaa mawe kumi na mawili kutoka katikati ya muto Yordani, jiwe moja kwa ajili ya kila kabila la Israeli, kama Yawe alivyomwambia Yoshua, wakaenda nayo mpaka pahali pale walipolala, wakayaweka kule.