Pahali pake, Mungu akawapitisha Waisraeli katika njia ya muzunguko kupitia katika jangwa, kuelekea bahari Nyekundu. Waisraeli wakaondoka katika inchi ya Misri wakiwa wamejitayarisha kwa vita.
Lakini kundi la waaskari la Wakaldea liliwafuatilia na kumukamata Zedekia karibu na Yeriko. Kisha kumukamata walimufikisha kwa Nebukadneza, mufalme wa Babeli huko Ribla, katika inchi ya Hamati, naye akamuhukumu.
Lakini sisi wenyewe tutatwaa silaha zetu tayari kwenda kwa vita pamoja na wandugu zetu Waisraeli, na tutakuwa kwa mustari wa mbele katika vita mpaka tuwafikishe pahali watakapokaa. Wakati huo watoto wetu watakaa kwenye miji yenye kuta, kwa kujilinda na wenyeji wa inchi hii.
“Wakati ule niliwapa maagizo haya: ‘Yawe, Mungu wenu amewapa inchi hii upande wa mashariki wa muto Yordani ikuwe mali yenu. Sasa ninyi mashujaa kati ya wandugu zenu, mutwae silaha muvuke muto Yordani mukiwa mbele ya wandugu zenu Waisraeli.
Katika siku hiyo Yawe akamutukuza Yoshua mbele ya Waisraeli wote, nao wakamuheshimu Yoshua maisha yake yote kama walivyomuheshimu Musa katika maisha yake.