Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Utawaamuru hao makuhani wanaobeba Sanduku la Agano wasimame karibu na ukingo wa muto Yordani wakati watakapofika kule.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 3:8
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Elia akamwambia Elisha: “Tafazali ubakie hapa. Yawe amenituma niende Yordani.” Lakini Elisha akasema: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, sitakuacha.” Basi, wakaenda pamoja.


Hawa wakawakusanya Walawi wenzao, wakajitakasa. Kisha wakaingia kama walivyotakiwa kufanya na mufalme, wakaanza kusafisha nyumba ya Yawe kama vile Yawe alivyoagiza.


Basi, Hezekia akaamuru sadaka ya kuteketeza kwa moto itolewe juu ya mazabahu. Mara tu sadaka hiyo ilipoanza kutolewa, watu wakaanza kumusifu Yawe kwa nyimbo zilizofuatana na mulio wa baragumu na vyombo vya muziki vya Daudi, mufalme wa Israeli.


Kisha mufalme Hezekia na viongozi wakawaambia Walawi wamusifu Yawe kwa nyimbo ambazo mufalme Daudi na nabii Asafu walizotunga. Basi, watu wote wakamutukuza Mungu kwa furaha, na kuinama uso mpaka chini.


Nguvu za Mungu zilikuwa zikifanya kazi katika Yuda, zikitia moyo wa kutii amri za mufalme na wakubwa wake kadiri ya maagizo ya Yawe.


Nikaagiza Walawi kujitakasa na kwenda kulinda milango kwa kutakasa siku ya Sabato. Ee, Mungu wangu, unikumbuke hata na kwa hili vilevile unihurumie kutokana na rehema zako kubwa.


Mumoja kati ya wana wa Yoyada mwana wa Kuhani Mukubwa Eliasibu, alioa binti wa Sanibalati kutoka muji wa Beti-Horoni, kwa sababu hiyo nikamufukuza kutoka mbele yangu.


Musa akawaambia Waisraeli: “Musiogope! Musimame imara! Leo mutaona jinsi Yawe atakavyowaokoa. Maana, hawa Wamisri munaowaona leo, hamutawaona tena.


Ni vizuri kwa mutu kungojea kwa utulivu wokovu unaotoka kwa Yawe.


Wakati Waisraeli walipokuwa wanavuka, makuhani waliokuwa wanalibeba Sanduku la Agano walisimama pahali pakavu katikati ya muto Yordani mpaka taifa lote likavuka.


wakawaambia watu: “Mutakapoliona Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, limebebwa na makuhani Walawi, mutaondoka na kulifuata;


Yawe akamwambia Yoshua: “Leo hii, nitaanza kukutukuza mbele ya watu wote wa Israeli kusudi wajue kwamba, kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo vilevile nitakavyokuwa pamoja nawe.


Kisha Yoshua akawaambia Waisraeli: “Musogee karibu mupate kusikia maneno ya Yawe, Mungu wenu.”


na watu wote walipokwisha kuvuka, wale makuhani wakawatangulia na lile Sanduku la Agano la Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ