Hawa wakawakusanya Walawi wenzao, wakajitakasa. Kisha wakaingia kama walivyotakiwa kufanya na mufalme, wakaanza kusafisha nyumba ya Yawe kama vile Yawe alivyoagiza.
Basi, Hezekia akaamuru sadaka ya kuteketeza kwa moto itolewe juu ya mazabahu. Mara tu sadaka hiyo ilipoanza kutolewa, watu wakaanza kumusifu Yawe kwa nyimbo zilizofuatana na mulio wa baragumu na vyombo vya muziki vya Daudi, mufalme wa Israeli.
Kisha mufalme Hezekia na viongozi wakawaambia Walawi wamusifu Yawe kwa nyimbo ambazo mufalme Daudi na nabii Asafu walizotunga. Basi, watu wote wakamutukuza Mungu kwa furaha, na kuinama uso mpaka chini.
Nikaagiza Walawi kujitakasa na kwenda kulinda milango kwa kutakasa siku ya Sabato. Ee, Mungu wangu, unikumbuke hata na kwa hili vilevile unihurumie kutokana na rehema zako kubwa.
Mumoja kati ya wana wa Yoyada mwana wa Kuhani Mukubwa Eliasibu, alioa binti wa Sanibalati kutoka muji wa Beti-Horoni, kwa sababu hiyo nikamufukuza kutoka mbele yangu.
Wakati Waisraeli walipokuwa wanavuka, makuhani waliokuwa wanalibeba Sanduku la Agano walisimama pahali pakavu katikati ya muto Yordani mpaka taifa lote likavuka.
Yawe akamwambia Yoshua: “Leo hii, nitaanza kukutukuza mbele ya watu wote wa Israeli kusudi wajue kwamba, kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo vilevile nitakavyokuwa pamoja nawe.