Kila mara karamu ilipomalizika, Yobu aliita wana wake kusudi awatakase. Aliamuka asubui mapema kisha karamu, akatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa ajili ya kila mumoja wao maana aliwaza: “Labda wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu ndani ya mioyo yao.”
Muwakusanye watu wote, muwatakase watu. Muwalete wazee, muwakusanye watoto, hata watoto wanaonyonya. Bwana-arusi na bibi-arusi watoke katika vyumba vyao.
Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.
Watu walizungukazunguka na kuikusanya, kisha waliisaga kwa mawe ya kusagia au waliitwanga katika vinu, halafu waliitokotesha ndani ya vyungu na kutengeneza maandazi. Onjo yake ilikuwa kama ya maandazi yaliyokaangwa kwa mafuta.
Wakati miguu ya makuhani wanaobeba Sanduku la Agano la Yawe, Bwana wa dunia yote, itakapoingia katika maji ya muto Yordani, maji ya muto huo yataacha kutiririka. Na yale yatakayokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yatajikusanya pamoja kama lundo.”
Na mara tu hao waliobeba Sanduku la Agano walipofika Yordani na miguu yao ilipokanyaga kwenye ukingo wa muto ule (muto Yordani unafurika wakati wa mavuno),
ndivyo mutakavyojua njia ya kupita maana hamujapita huku hata kidogo. Lakini musilikaribie sana Sanduku la Agano; mukuwe kwa umbali wa kilometre moja hivi.”
Basi, simama uwatakase watu, uwaambie wajitakase na kujitayarisha kwa siku ya kesho, maana mimi Yawe, Mungu wa Israeli, ninasema hivi: ‘Kati yenu kuna vitu vilivyotolewa viangamizwe. Hamuwezi kuwashinda waadui zenu mpaka vitu hivyo vimeondolewa kati yenu!
Samweli akawajibu: “Nimekuja kwa amani. Nimekuja kumutolea Yawe sadaka. Mujitakase wenyewe halafu tuende kutolea sadaka.” Samweli akamutakasa Yese pamoja na wana wake, akawakaribisha kwenye sadaka.