Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 wakawaambia watu: “Mutakapoliona Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, limebebwa na makuhani Walawi, mutaondoka na kulifuata;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 3:3
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wale waliolibeba Sanduku la Yawe kila mara walipopiga hatua sita, Daudi alitoa sadaka: ngombe dume na mwana-ngombe mumoja wenye kunona.


Basi, wakaondoa Sanduku la Mungu kutoka katika nyumba ya Abinadabu iliyokuwa juu ya mulima, wakalibeba juu ya gari jipya. Wana wa Abinadabu, Uza na Ahio, wakaongoza gari lile jipya,


Kisha kufika kwa wazee wote wa Israeli, makuhani walibeba Sanduku la Agano.


Vilevile nao makuhani wa ukoo wa Lawi watakuwa pale siku zote kwa kunitumikia wakinitolea sadaka za kuteketezwa na sadaka za unga na kunitolea sadaka milele.


Basi, watu wakasafiri toka Sinai, mulima wa Yawe, mwendo wa siku tatu. Sanduku la Agano la Yawe liliwatangulia mwendo wa siku tatu, kwa kuwatafutia pahali pa kupigia kambi.


Kisha Haruni na wana wake kufunika Pahali Patakatifu pamoja na vyombo na vifaa vyake vyote, wakiwa tayari kuanza safari, watu wa ukoo wa Kohati watakuja na kuvibeba. Lakini wao, hawaruhusiwi kabisa kugusa vyombo hivyo vitakatifu, kusudi wasikufe. Hiyo ndiyo kazi ya ukoo wa Kohati kila wakati hema la mukutano linapohamishwa.


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kama mutu akitaka kunifuata, ajikane yeye mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.


Mwalimu mumoja wa Sheria akamufikia na kumwambia: “Mwalimu, nitakufuata popote utakapokwenda.”


akawaambia Walawi waliokuwa wanabeba lile Sanduku la Agano la Yawe:


Basi, Musa akaandika sheria hiyo, akawapa makuhani wa ukoo wa Lawi ambao walikuwa wakibeba Sanduku la Agano la Yawe, na wazee wote wa Israeli.


ndivyo mutakavyojua njia ya kupita maana hamujapita huku hata kidogo. Lakini musilikaribie sana Sanduku la Agano; mukuwe kwa umbali wa kilometre moja hivi.”


Kisha akawaambia makuhani: “Mutwae Sanduku la Agano, mutangulie nalo mbele ya watu.” Nao wakalitwaa na kutangulia mbele ya watu.


Utawaamuru hao makuhani wanaobeba Sanduku la Agano wasimame karibu na ukingo wa muto Yordani wakati watakapofika kule.”


Wale makuhani waliobeba Sanduku la Agano, walisimama katikati ya muto Yordani mpaka watu walipomaliza kutimiza kila kitu ambacho Yawe alimwamuru Yoshua awaambie watu; Yoshua alifanya yote ambayo Musa alikuwa amemwamuru. Watu wakaharakisha kuvuka muto,


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawaita makuhani, akawaambia: “Mulibebe Sanduku la Agano na makuhani saba watwae mabaragumu saba ya kondoo dume, watangulie mbele ya Sanduku la Yawe.”


Watu wale ndio waliojilinda katika usafi bila kujichafua kwa kulala na wanawake, nao wanamufuata Mwana-Kondoo kila fasi anapokwenda. Wamekombolewa kati ya watu wengine kusudi wakuwe wa kwanza kutolewa kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo kama vile sadaka ya mavuno ya kwanza.


Walawi walikuwa wameliteremusha Sanduku la Yawe na kile kibweta chenye sanamu za zahabu na kuziweka kwenye lile jiwe kubwa. Basi, siku hiyo watu wa Beti-Semesi walitoa sadaka za kuteketezwa, na kumutolea Yawe sadaka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ