Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 3:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 maji yaliyokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yalisimama na kulundikana mpaka kule Adamu kijiji kinachokuwa karibu na muji wa Zaretani. Maji yaliyokuwa yanateremuka kwenda katika bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, yalitoweka kabisa, watu wakavuka mbele ya Yeriko.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 3:16
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wafalme wale watano waliyaunganisha majeshi yao katika bonde la Sidimu, ni kusema bahari ya Chumvi.


Vitu hivyo vyote mufalme alivitengeneza katika kiwanda cha Yordani, sehemu ya udongo wa mufinyanzi iliyokuwa kati ya Sukoti na Zaretani.


Bahari iliona hayo ikakimbia; muto Yordani ukaacha kutiririka!


Ee bahari, nini iliyokufikia hata ukakimbia? Nawe Yordani, kwa nini uliacha kutiririka?


Yawe ameikaa juu ya mafuriko ya maji; Yawe ni mufalme anayetawala milele.


Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa, akavifunga vilindi vya bahari ndani ya gala.


Aligeuza bahari kuwa inchi kavu, watu wakapita humo kwa miguu; kwa hiyo nasi tukashangilia.


Wewe umefanya chemichemi na vijito; na kukausha mito mikubwa.


Kishindo cha ngurumo yako kilitokea katika zoruba, umeme wako ukaangaza ulimwengu, dunia ikatikisika na kutetemeka.


Aligawanya bahari, akawapitisha ndani yake; aliyafanya maji yasimame kama ukuta.


Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari, naye Yawe akasukuma bahari nyuma kwa upepo mukali toka upande wa mashariki. Upepo ule ulivuma usiku kucha, ukagawanya bahari sehemu mbili na katikati kukatokea inchi kavu.


Waisraeli wakapita katikati ya bahari pahali pakavu, kuta za maji zikiwa upande wao wa kuume na wa kushoto.


Lakini Waisraeli walipita katikati ya bahari pahali pakavu, kuta za maji zikiwa zimesimama upande wao wa kuume na wa kushoto.


Kwa pumzi ya pua yako maji yalilundikana, mawimbi yakasimama wima kama ukuta; vilindi katikati ya bahari vikagandamana.


Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.


Akaniambia: Maji haya yanatiririka kupitia katika inchi mpaka katika bonde la Yordani, na yakifika huko yatayafanya maji ya bahari ya Chumvi kuwa maji mazuri.


Anaikaripia bahari na kuikausha, yeye anaikausha mito yote. Mbuga za Basani na mulima Karmeli zinanyauka, maua ya Lebanoni yanakauka.


Ee Yawe, umeikasirikia mito? Umeyakasirikia maji ya bahari? Ulipanda juu ya gari lako la vita na kuendesha farasi kwa kupata ushindi.


Upande wa kusini mupaka wenu utakuwa kutoka jangwa la Sini kupitia upande wa Edomu. Utaanzia mashariki upande wa kusini mwisho wa bahari ya Chumvi.


Kitabu hiki kina maneno ambayo Musa aliwaambia watu wote wa Israeli wakati walipokuwa katika jangwa upande wa mashariki wa muto Yordani. Walikuwa katika bonde la Yordani karibu na Sufu, kati ya muji wa Parani upande mumoja na miji ya Tofeli, Labani, Hazeroti na Dizahabu upande mwingine.


Upande wa magaribi, inchi yao ilienea mpaka muto Yordani. Toka ziwa Galilaya upande wa kaskazini, ukashuka mpaka kwenye bahari ya Araba, ni kusema bahari ya Chumvi, mpaka kwenye miteremuko ya Pisiga, upande wa mashariki.


Vilevile, alitawala inchi yote ya Araba, kutokea bahari ya Kineroti, upande wa mashariki, mpaka Beti-Yesimoti kwenye bahari ya Chumvi na kuendelea mpaka chini ya mulima Pisiga.


Mupaka wao upande wa kusini ulianzia kwenye pembe ya kusini ya bahari ya Chumvi,


Kutoka Yanoa ulikwenda hata Ataroti na Nara, hata kufika Yeriko, ambako uliishia katika muto Yordani.


Wakati miguu ya makuhani wanaobeba Sanduku la Agano la Yawe, Bwana wa dunia yote, itakapoingia katika maji ya muto Yordani, maji ya muto huo yataacha kutiririka. Na yale yatakayokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yatajikusanya pamoja kama lundo.”


Mutawaambia hivi: ‘Taifa la Israeli lilivuka muto huu wa Yordani pahali pakavu.’


Wafalme wote wa Waamori walioishi ngambo ya magaribi ya Yordani, na wafalme wote wa Wakanana waliokuwa kandokando ya bahari ya Mediteranea, waliposikia kwamba Yawe aliyakausha maji ya muto Yordani kwa ajili ya Waisraeli mpaka walipokwisha kuvuka, wakavunjika moyo; wakaishiwa nguvu kabisa kwa kuwaogopa Waisraeli.


Watu wa Gideoni walipopiga baragumu zao mia tatu, Yawe akawafanya Wamidiani waanze kuuana wao kwa wao katika kambi. Waliobaki wakatoroka mpaka Zerera, wakafika Beti-Sita, hata kwenye mupaka wa Abeli-Mehola karibu na Tabati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ