Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 3:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Wakati miguu ya makuhani wanaobeba Sanduku la Agano la Yawe, Bwana wa dunia yote, itakapoingia katika maji ya muto Yordani, maji ya muto huo yataacha kutiririka. Na yale yatakayokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yatajikusanya pamoja kama lundo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 3:13
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote.


Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa, akavifunga vilindi vya bahari ndani ya gala.


Wewe umefanya chemichemi na vijito; na kukausha mito mikubwa.


Aligawanya bahari, akawapitisha ndani yake; aliyafanya maji yasimame kama ukuta.


Kwa pumzi ya pua yako maji yalilundikana, mawimbi yakasimama wima kama ukuta; vilindi katikati ya bahari vikagandamana.


Muumba wako atakuwa mume wako. Jina lake Yawe wa majeshi. Mukombozi wako ni Mutakatifu wa Israeli. Yeye anaitwa Mungu wa Ulimwengu Wote.


Kwa farasi wako ulitembea juu ya bahari, bahari inayosukwasukwa na mawimbi.


Halafu akaniambia: Hawa ndio wale watu wawili ambao Bwana wa ulimwengu wote aliwachagua kwa kuwapakaa mafuta kusudi wamutumikie.


Muangalie, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote liko karibu kupita mbele yenu kuelekea muto Yordani.


Ninyi mutawaambia: ‘Sanduku la Agano la Yawe lilipopitishwa katika muto Yordani, maji ya muto huo yalizuiliwa yasitiririke!’ Kwa hiyo mawe haya yatakuwa ukumbusho kwa Waisraeli milele.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ