Yoshua 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Asubui mapema Yoshua pamoja na watu wote wa Israeli walianza safari kutoka Sitimu. Walipofika kwa muto Yordani, walipiga kambi hapo kwa muda mbele ya kuvuka.
Hivyo, asubui mapema, Abrahamu akatwaa chakula na chupa la maji, akamupa Hagari na kumubebesha mutoto juu ya bega. Akamufukuza pamoja na mwana wake. Hagari akaondoka, akakuwa anatangatanga katika jangwa la Beri-Seba.
Basi, kesho yake, Abrahamu akaamuka asubui mapema, akatandika punda wake, akawatwaa watumishi wake wawili pamoja na Isaka mwana wake. Akatayarisha kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto, kisha akaanza safari kuelekea pahali alipoambiwa na Mungu.
Kwa muda wa miaka makumi mbili na tatu sasa, ni kusema tangu mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa mufalme Yosia, mufalme wa Yuda, mwana wa Amoni, mpaka hivi leo, nimekuwa nikipata neno la Mungu na kulitoa kwenu kila wakati, lakini ninyi hamukusikiliza.
Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!
Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kwa siri kutoka Sitimu waende kufanya upelelezi katika inchi ile na hasa muji wa Yeriko. Wakaenda, wakafika kwenye nyumba ya kahaba mumoja aliyeitwa Rahabu wakalala humo.
Kesho yake, Daudi aliamuka asubui mapema, na akamwachia muchungaji mumoja kondoo. Alibeba chakula na kwenda kama vile alivyoagizwa na baba yake Yese. Alipofika kwenye kambi ya Waisraeli, aliwakuta wanajipanga kwenye sehemu yao ya vita na wanapiga kelele za vita.