Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 24:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kisha niliwaongoza mpaka katika inchi ya Waamori ambao waliishi upande mwingine wa muto Yordani. Walipigana nanyi, lakini mimi niliwapa ushindi juu yao mukawaangamiza na kuiteka inchi yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 24:8
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ukawapatia ushindi juu ya falme na mataifa, ukawafanyia mengi kila upande. Wakashinda inchi ya Hesiboni iliyotawaliwa na mufalme Sihoni; na tena wakashinda inchi ya Basani iliyotawaliwa na mufalme Ogi.


Malaika wangu atakapowaongoza na kuwafikisha katika inchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanana, Wahivi na Wayebusi, nami nitawaangamiza wale wote.


Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.


Hata hivyo, enyi watu wangu, kwa ajili yenu, niliwaangamiza kabisa Waamori ambao walikuwa wakubwa kama mierezi, wenye nguvu kama miti ya mialo. Niliwaangamiza, matawi na mizizi.


Kisha Sihoni akatoka na watu wake wote kupigana nasi karibu na muji wa Yahasa.


pamoja na miji ya mufalme Sihoni wa Waamori, aliyetawala kule Hesiboni hata kwa mupaka wa Waamoni,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ