Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 24:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Naye Eleazari mwana wa Haruni, akakufa na kuzikwa Gibea, muji ambao mwana wake Finehasi alikuwa amepewa katika inchi ya milima ya Efuraimu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 24:33
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ulivyosema si kweli! Lakini mutu mumoja kutoka sehemu ya milima ya Efuraimu anayeitwa Seba mwana wa Bikiri anataka kumwasi mufalme Daudi. Mumutoe kwangu nami nitaondoka katika muji wenu.” Yule mwanamuke akamwambia Yoabu: “Kichwa chake kitarushwa kwako kupitia juu ya ukuta.”


Haya ndiyo majina ya hao maliwali: Beni-Huri alisimamia sehemu ya milima ya Efuraimu. Beni-Dekari alisimamia miji ya Makasi, Salabimu, Beti-Semesi na Eloni-Beti-Hanani. Beni-Hesedi alisimamia muji wa Aruboti, alisimamia vilevile Soko na inchi yote ya Heferi. Beni-Abinadabu, mume wa Tafati, binti ya Solomono, alisimamia jimbo lote la Dori. Bana mwana wa Ahiludi, alisimamia miji ya Tanaki, Megido, na sehemu yote ya Beti-Seani inayokuwa karibu na muji wa Zaretana, upande wa kusini wa muji wa Yezereheli, na kutoka Beti-Seani mpaka miji ya Abeli-Mehola, na hata kupita muji wa Yokimamu. Beni-Geberi alisimamia muji wa Ramoti-Gileadi pamoja na vijiji vya Gileadi vilivyokuwa vya Yairi mwana wa Manase; tena alisimamia jimbo la Argobu katika inchi ya Basani; yote kwa jumla ilikuwa miji mikubwa makumi sita iliyozungushiwa kuta na kuwekwa vifungio vya shaba kwenye mulango. Ahinadabu mwana wa Ido, alisimamia jimbo la Mahanaimu. Ahimasi, mume wa Basemati, binti ya Solomono, alisimamia sehemu ya inchi ya Nafutali. Bana mwana wa Husayi, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Aseri na Bealoti. Yosafati mwana wa Parua, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Isakari. Simei mwana wa Ela, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Benjamina. Geberi mwana wa Uri, alisimamia sehemu ya inchi ya watu wa kabila la Gileadi, ambayo zamani ilitwaliwa na Sihoni mufalme wa Waamori, na Ogu mufalme wa Basani. Zaidi ya hawa kumi na wawili, kulikuwa mukubwa mumoja aliyesimamia inchi nzima ya Yuda.


Gehazi akajibu: “Mambo yote ni sawa lakini tu bwana wangu amenituma nikuambie kwamba sasa hivi amepokea watu wawili wa kundi la manabii katika inchi ya milima ya Efuraimu, naye angependa uwape vikoroti elfu tatu vya feza na nguo mbili ya sikukuu.”


mwana wa Abisua mwana wa Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni, Kuhani Mukubwa.


Kweli! Ninajua utanipeleka tu katika kifo, pahali wote wanaoishi watakapokutana.


kimwezeshe aendelee kuishi siku zote, bila kuona kaburi.


Haruni alimwoa Eliseba, binti ya Aminadabu, dada ya Nasoni; naye akamuzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.


Eleazari mwana wa Haruni, alimwoa mumoja wa wabinti za Putieli, naye akamuzalia Finehasi. Hawa ndio waliokuwa wakubwa wa jamaa za Lawi.


Babu zenu, wako wapi? Na manabii, wanaishi milele?


Naye Eleazari mwana wa kuhani Haruni aliwekwa kuwa mukubwa wa wakubwa wa Walawi, na musimamizi wa watumishi wote wa Pahali Patakatifu.


Lakini Daudi alipokwisha kutumika sawasawa na kusudi la Mungu katika maisha yake, akakufa na kwenda kukutana na babu zake waliomutangulia, naye akaoza.


Lakini Yesu hawezi kukombolewa kwa kazi yake ya ukuhani, kwa sababu yeye anaishi kwa milele.


Haya ndiyo maeneo ya inchi ambayo Waisraeli walipewa katika inchi ya Kanana. Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, pamoja na wakubwa wa ukoo za makabila ya Waisraeli waliyowagawanyia Waisraeli.


Basi, watu wa Israeli wakamutuma Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, kule Gileadi kwa makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase.


Kijana huyo akaondoka Betelehemu katika inchi ya Yuda, akaenda kutafuta pahali pengine pa kuishi. Katika safari yake akafika katika nyumba ya Mika katika inchi ya milima ya Efuraimu.


Kutoka kule wakaelekea inchi ya milima ya Efuraimu, wakafika katika nyumba ya Mika.


Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni alikuwa na kazi ya kutumika mbele yake. Waisraeli wakamwuliza Yawe: “Twende tena kupigana na wandugu zetu, watu wa kabila la Benjamina?” Yawe akawaambia: “Muende. Kesho nitawatia katika mikono yenu.”


Kulikuwa mutu mumoja katika muji wa Rama katika inchi ya milima ya Efuraimu jina lake Elekana wa kabila la Efuraimu. Yeye alikuwa mwana wa Yerohamu, na mujukuu wa Elihu mwana wa Tohu mwana wa Zufu.


Wakawatafuta kwenye inchi ya milima ya Efuraimu na eneo la Shalisa, lakini hawakuwaona kule. Halafu wakafika Salimu, na kule hawakuwaona. Wakawatafuta katika inchi ya Benjamina, hata hivyo hawakuwapata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ