Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 24:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Halafu akawaambia watu wote: “Jiwe hili ndilo litakalokuwa ushuhuda kwetu, maana limesikia maneno yote ambayo Yawe ametuambia. Kwa hiyo, litashuhudia juu yenu, kusudi musipate kumwasi Mungu wenu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 24:27
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana hasara kutoka kwa Mungu ni kitisho kwangu; mimi siwezi kusimama mbele ya ukubwa wake.


Huo ungekuwa uovu wa kuazibiwa na waamuzi maana ningekuwa mwongo mbele ya Mungu anayekuwa juu.


maana nikipata mali mengi nitakusahau; nikisema: “Yawe ni nani?” Au nikiwa masikini nitaiba, na kuzaraulisha jina lako ee Mungu wangu.


Yawe anasema hivi: Sikiliza enyi mbingu, tega sikio ee dunia. Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha, lakini sasa wameniasi!


Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.


Ndiyo maana hata mawe yatalalamika juu ya ukuta, na miti ya nyumba itayaunga mukono.


lakini kwa muda wa mwezi muzima! Mutaikula mpaka iwatoke ndani ya pua, mpaka muichukie. Yote hayo ni kwa sababu mumemukataa Yawe anayekuwa hapahapa kati yenu, na kulia mbele yake mukisema: Kwa nini tulitoka Misri?


Lakini kila mutu anayenikana mbele ya watu, nami nitamukana vilevile mbele ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Yesu akawajibu: “Ninawaambia ninyi: kama watu hawa wakinyamaza, mawe yatalalamika.”


Ninaita mbingu na inchi zishuhudie juu yenu leo hii, kwamba nimewapa uchaguzi kati ya uzima na kifo, kati ya baraka na laana. Basi, muchague uzima ninyi na wazao wenu mupate kuishi.


“Sasa, andika wimbo huu, uwafundishe watu wa Israeli kusudi ukuwe ushuhuda wangu juu yao.


Watakapopatwa na hasara nyingi na taabu, wimbo huu utakuwa kama ushuhuda maana hautasahauliwa na wazao wao. Hata sasa, mbele sijawapeleka katika inchi niliyoapa kuwapa, ninajua mipango ambayo wanapanga.”


“Mutwae kitabu hiki cha sheria, mukiweke karibu na Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, kusudi kikuwe ushuhuda juu yenu.


Utege sikio, ee mbingu. Sikiliza, ee dunia, maneno ninayosema.


Wanajidai kwamba wanamujua Mungu, lakini wanamukana kwa matendo yao. Wao ni wenye machukizo, waasi hata hawafai kwa kufanya kazi yo yote nzuri.


Watu wa makabila ya Rubeni na Gadi wakaiita ile mazabahu “Ushuhuda”, maana walisema: “Mazabahu hii ni ushuhuda wetu kwamba Yawe ndiye Mungu.”


Halafu Yoshua akawaruhusu watu waondoke; nao wakaenda kila mumoja kwake.


Ninajua matendo yako. Ninajua kwamba wewe hauna uwezo mwingi, lakini umeshika neno langu, nawe haukukana jina langu. Basi nimefungua mulango wazi mbele yako, wala hakuna anayeweza kuufunga.


Kisha, Samweli alitwaa jiwe na kulisimamisha kati ya Misipa na Seni, akaliita jiwe hilo “jiwe la musaada”, akisema: “Yawe ametusaidia mpaka sasa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ