Basi, wakamupa Yakobo sanamu zote za miungu ya kigeni walizokuwa nazo pamoja na pete walizokuwa wamevaa kwa masikio. Na Yakobo akavizika chini ya muti wa mwalo uliokuwa karibu na Sekemu.
Watu wote wa Yuda walikuwa na furaha tele kwa sababu walikuwa wameapa kwa moyo wote. Walikuwa wamemutafuta kwa hamu, wakamupata. Naye Yawe akawapa amani pande zote.
Halafu Musa akamulilia Yawe, naye akamwonyesha kipande cha muti, na Musa akakitumbukiza katika maji. Maji hayo yakakuwa mazuri. Kule Mungu aliwapa Waisraeli sharti na agizo, kusudi awapime,
Basi, Musa akaenda na kuwaambia watu wote maneno na maagizo yote Yawe aliyomwambia. Watu wote wakajibu kwa sauti moja: Mambo yote Yawe aliyosema, tutayafanya.
Musa akawaita pamoja Waisraeli wote akawaambia: “Muliona ninyi wenyewe jinsi Yawe alivyomutendea mufalme wa Misri, wakubwa, watumishi wake na inchi yake yote.
Kisha Yoshua akayakusanya makabila yote ya Waisraeli kule Sekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na wakubwa wa Waisraeli, nao wakakuja mbele ya Mungu.