22 Halafu Yoshua akawaambia: “Ninyi ni washuhuda wenu wenyewe kwamba mumechagua kumutumikia Yawe.” Nao wakamujibu: “Sisi ni washuhuda.”
Maneno yako mwenyewe yanakuhukumu, sio mimi; masemi yako yanashuhudia juu yako.
Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.
Ukuwe siku zote tayari kunisaidia, maana nimeamua kufuata kanuni zako.
Kuna kitu kimoja tu cha lazima. Maria amechagua kitu kinachokuwa kizuri zaidi ambacho hakuna mutu atakayekiondoa kwake.”
Yule bwana akamujibu: ‘Wewe mutumishi mubaya! Nitakuhukumu kufuatana na maneno yako. Ulijua kama mimi ni mutu mugumu, ninayetafutia nafasi nisipowekea na kuvuna nafasi nisipopanda.
Leo Yawe ameahidi kwamba atakuwa Mungu wenu, kama mutafuata njia zake na kushika masharti, amri, na maagizo yake na kutii sauti yake.
Nao watu wakamwambia Yoshua: “Hapana! Sisi tutamutumikia Yawe tu.”