Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 24:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini Yoshua akawaambia: “Ninyi hamuwezi kumutumikia Yawe, maana yeye ni Mungu Mutakatifu. Yeye ni Mungu mwenye wivu, naye hatawasamehe makosa na zambi zenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 24:19
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Wote wasifu jina lake kubwa la kutisha. Yeye ni mutakatifu!


Mumusifu Yawe, Mungu wetu; muiname uso mpaka chini mbele yake. Yeye ni mutakatifu!


Mumusifu Yawe, Mungu wetu; muiname kwa mulima wake mutakatifu! Yawe, Mungu wetu, ni mutakatifu.


Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.


Musikilize na kutii maneno atakayosema, wala musimwasi. Hatawasamehe uasi wenu maana nimemutuma kwa jina langu.


Musiabudu mungu yeyote mwingine, maana mimi Yawe ninajulikana kwa jina: Mwenye Wivu. Mimi ni Mungu mwenye wivu.


Anawatendea mema maelfu, anawasamehe uovu, makosa na zambi. Lakini hataacha kumwazibu mwenye kosa. Anawalipiza watoto na wajukuu uovu wa baba na babu zao, hata kizazi cha tatu na cha ine.


Kwa hiyo, kila mutu atapata haya na kufezeheshwa. Usiwasamehe hata kidogo, ee Mungu!


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Mugeuke na kuiacha njia ya ukweli; musituambie tena juu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.


Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.


Lakini Yawe wa majeshi anatukuzwa wakati sheria yake inafuatwa. Utakatifu wa Mungu Mutakatifu unaonyeshwa wakati haki inatendwa.


Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.


Kwa sababu mimi ni Yawe, Mungu wenu, mujitakase na kuwa watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu. Wala musijichafue na kitu chochote kinachotambaa juu ya inchi.


Kwa sababu ni mimi Yawe niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu; kwa hiyo mukuwe watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu.


Uwaambie Waisraeli wote pamoja hivi: Mukuwe watakatifu maana mimi Yawe, Mungu wenu, ni mutakatifu.


Kwa sababu mimi Yawe ni mutakatifu, nami nimewatenga ninyi na mataifa mengine kusudi mukuwe mali yangu, mutakuwa watakatifu.


Kwa hiyo, mujitakase mukuwe watakatifu, maana mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Yawe ni Mungu mwenye wivu, anayelipiza kisasi; Yawe analipiza kisasi na ni mwenye kasirani; Yawe analipiza kisasi kwa wapinzani wake, kasirani yake inawaka juu ya waadui zake.


Wewe ni mutakatifu kabisa, hauwezi kutazama uovu, hauwezi kuvumilia hata kidogo kuona mabaya. Mbona basi unawaona wafanya maovu na kunyamaza, kwa nini unanyamaza waovu wanapowamaliza wale watu wanaokuwa wenye haki kuliko wao?


“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.


“Yawe alituondolea watu wote, ni kusema Waamori wote waliokaa katika inchi. Kwa hiyo, nasi tutamutumikia Yawe, maana ndiye Mungu wetu.”


Naye akawaambia: “Basi, muondoe miungu ya kigeni munayokuwa nayo, mumufuate Yawe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wenu wote.”


Basi Naomi akamwambia: “Ruta, angalia dada yako amerudi kwao na kwa mungu wake; basi, nawe vilevile urudi, umufuate dada yako.”


Kwa hiyo ninaapa juu ya jamaa ya Eli kwamba uovu wao hautaondolewa hata kidogo kwa matoleo wala kwa sadaka.”


Kisha, wakaaji wa muji wa Beti-Semesi wakasema: “Nani anayeweza kusimama mbele ya Yawe, huyu Mungu mutakatifu? Atakwenda kwa nani kusudi aondoke kwetu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ