Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 24:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 “Yawe alituondolea watu wote, ni kusema Waamori wote waliokaa katika inchi. Kwa hiyo, nasi tutamutumikia Yawe, maana ndiye Mungu wetu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 24:18
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, mimi ni mutumishi wako, mutumishi wako, mutoto wa mujakazi wako. Umenifungulia vifungo vyangu.


na ninyi mupate kuwaelezea watoto wenu na wajukuu wenu jinsi nilivyowachekelea Wamisri kwa kuonyesha vitambulisho vile kati yao. Hivyo mutatambua kwamba mimi ni Yawe.”


Yawe ananijalia nguvu na uwezo, yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. Yeye ni Mungu wangu nami nitamusifu; ni Mungu wa baba yangu nami nitamutukuza.


Mipaka ya inchi yenu itakuwa kutoka bahari Nyekundu mpaka bahari ya Mediteranea na kutoka jangwa mpaka muto Furati. Nitawatia wakaaji wa inchi ile katika mikono yenu, nanyi mutawafukuza wawaondokee.


mataifa mengi yataufikia na kusema: Tuende juu kwenye mulima wa Yawe, tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo, kusudi atufundishe njia zake, nasi tuzifuate. Maana sheria itatoka kule Sayuni; na neno la Yawe kule Yerusalema.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Wakati ule, watu kumi kutoka mataifa ya kila luga watamukamatilia Muyuda mumoja na kushika nguo yake na kumwambia: Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa sababu tumesikia kwamba Mungu yuko pamoja nanyi.


Kisha ile hema ikaachwa kwa kizazi cha babu zetu kilichofuata. Nao wakaibeba chini ya uongozi wa Yoshua mpaka waliponyanganya inchi ya mataifa yale Mungu aliyofukuza mbele ya kufika kwao. Nayo ikabaki katika inchi mpaka katika siku za Daudi.


Yeye ni utukufu wenu. Yeye ni Mungu wenu ambaye amewatendea haya mambo makubwa na ya kutisha muliyoona kwa macho yenu wenyewe.


Mungu wa milele ndiye kimbilio lenu; nguvu yake inaonekana katika dunia. Aliwafukuza waadui mbele yenu; aliwaamuru: ‘Muwaangamize.’


Maana Yawe ameyafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu na hakuna mutu ambaye ameweza kuwapinga ninyi mpaka leo.


Maana, Yawe, Mungu wetu, ndiye aliyetutoa sisi pamoja na wazee wetu katika inchi ya Misri tulikokuwa watumwa, tukayaona kwa macho yetu wenyewe matendo ya ajabu aliyotenda. Akatulinda katika safari zetu zote na kati ya watu wote ambao tulipita kati yao.


Lakini Yoshua akawaambia: “Ninyi hamuwezi kumutumikia Yawe, maana yeye ni Mungu Mutakatifu. Yeye ni Mungu mwenye wivu, naye hatawasamehe makosa na zambi zenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ