Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 24:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Maana, Yawe, Mungu wetu, ndiye aliyetutoa sisi pamoja na wazee wetu katika inchi ya Misri tulikokuwa watumwa, tukayaona kwa macho yetu wenyewe matendo ya ajabu aliyotenda. Akatulinda katika safari zetu zote na kati ya watu wote ambao tulipita kati yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 24:17
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Lakini kwa ngambo yetu, Yawe ni Mungu wetu, wala hatujamwacha. Tena tuko na makuhani wa uzao wa Haruni ambao wanamutumikia Yawe, nao wanasaidiwa na Walawi.


Kama kisha mwana wako akiuliza maana ya jambo hili, utamwambia: ‘Kwa nguvu ya mukono wake, Yawe alitutoa katika inchi ya Misri ambako tulikuwa watumwa.


Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.


‘Ninyi wenyewe mumeona jinsi nilivyowatendea Wamisri na jinsi nilivyowapeleka ninyi kama vile tai anavyopeleka watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu.


Mimi nitabaki yuleyule hata katika uzee wenu; hata katika wakati wenu wa imvi mimi nitawabeba. Nilifanya hivyo kwanza, nitafanya hivyo tena. Nitawabeba ninyi na kuwaokoa.


Muliona majaribu makubwa, vitambulisho na maajabu aliyotenda.


lakini alijiwekea watu wa Yakobo kuwa wake, hao alijichagulia kuwa mali yake.


Mukumbuke ugonjwa mukali muliouona kwa macho yenu, miujiza na maajabu na nguvu kubwa na uwezo mukubwa, ambavyo Yawe, Mungu wenu alitumia kwa kuwakomboa; vile ndivyo atakavyowatendea watu munaowaogopa.


Halafu watu wakamujibu: “Hatutaweza hata kidogo kumwacha Yawe na kuitumikia miungu mingine.


“Yawe alituondolea watu wote, ni kusema Waamori wote waliokaa katika inchi. Kwa hiyo, nasi tutamutumikia Yawe, maana ndiye Mungu wetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ