Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 24:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 24:15
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


Basi, Yakobo akawaambia jamaa yake na wote aliokuwa nao: “Mutupilie mbali sanamu za miungu ya kigeni munazokuwa nazo, mujitakase na kubadilisha nguo zenu.


Kisha, Elia akawakaribia watu hao, akawaambia: “Mutaendelea kusitasita ndani ya mioyo mpaka wakati gani? Ikiwa Yawe ni Mungu, mumufuate; lakini ikiwa Bali ni Mungu, basi, mumufuate.” Lakini watu hawakumujibu neno lolote.


Kanana vilevile ndiye babu ya Wayebusi, Waamori, Wagirgasi,


Nitashikamana na mwenendo mukamilifu. Utakuja kwangu wakati gani? Nitaishi kwa ukamilifu ndani ya nyumba yangu;


Nimeapa na kuhakikisha kiapo changu, kwamba nitashika maamuzi yako ya haki.


Usifuate watu wengi kwa kutenda ubaya. Wala wakati wa kukata maneno, usishuhudie kufuatana na watu wengi kwa kupotosha haki.


Musiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala musiige mambo yao. Lakini mutawaangamiza kabisa na kuvunjavunja nguzo zao.


Musifanye mapatano yoyote na wakaaji wa inchi hiyo, maana watakapoabudu miungu yao ya uongo na kuitambikia, watawaalika, nanyi mutashawishiwa kula vyakula wanavyotambikia miungu yao.


Na sasa, enyi Waisraeli, Bwana wenu Yawe anawaambia hivi: Muendelee kuziabudu sanamu zenu za miungu, kama hamunisikilizi; lakini mutalazimishwa kuacha kulikufuru jina langu takatifu kwa sadaka na sanamu zenu.


Lakini, hata kama haitafanyika hivyo, ujue wazi, ee mufalme, kwamba sisi hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya zahabu uliyosimamisha.


Kisha watatwaa mawe mapya na kujenga pahali walipobomoa. Nao watapiga nyumba hiyo lipu upya.


Mataifa mengine yanafuata njia zao, kwa kuitegemea miungu yao, lakini sisi tunafuata njia zetu kwa kumutegemea Yawe, Mungu wetu, milele na milele.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


“Ikiwa ndugu yako wa tumbo moja, au mwana wako, au binti wako, au muke wako unayemupenda sana au rafiki yako mupenzi, atakushawishi kwa siri akisema: ‘Twende tuabudu miungu mingine’, ambayo wewe wala babu zenu hamwijui,


Kisha kusikia maneno ya agano hili ambayo mumeapishwa, na mutu akijiamini mwenyewe ndani ya moyo wake na kusema atakuwa salama naye akifuata ugumu wake, hiyo italeta maangamizi.


Halafu watu wakamujibu: “Hatutaweza hata kidogo kumwacha Yawe na kuitumikia miungu mingine.


Kisha nikawakumbusha kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, na kwamba musiiheshimu miungu ya Waamori, ambao inchi yao mumeitwaa, lakini hamukuisikiliza sauti yangu.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ