Yoshua 24:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Kisha Yoshua akayakusanya makabila yote ya Waisraeli kule Sekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na wakubwa wa Waisraeli, nao wakakuja mbele ya Mungu.
Abramu akapita katikati ya inchi mpaka Sekemu, pahali patakatifu, penye muti wa mwelo wa More. Wakati ule, Wakanana walikuwa ndio wenyeji wa inchi hiyo.
Basi, wakamupa Yakobo sanamu zote za miungu ya kigeni walizokuwa nazo pamoja na pete walizokuwa wamevaa kwa masikio. Na Yakobo akavizika chini ya muti wa mwalo uliokuwa karibu na Sekemu.
Na pale pale nikatuma watu kwako, nawe umefanya vizuri kwa kufika. Sasa sisi wote tuko hapa mbele ya Mungu kwa kusikiliza mambo yote Bwana aliyokuagiza kutuambia.”
Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.
Watu wote wa jeshi la Waisraeli wakaenda Beteli. Wakaikaa kule mbele ya Yawe wakiomboleza na kufunga mpaka magaribi. Wakamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.
Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”