Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 23:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Lakini kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyotimiza mambo yote mema aliyowaahidi, ni vile vile anavyoweza kuwaletea maovu yote mpaka awaangamize wote kutoka inchi hii nzuri ambayo amewapa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 23:15
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hakika, tangu sasa, Yawe atawapiga watu wa Israeli, nao watatikisika kama unyasi unavyotikiswa ndani ya muto. Atawaongoa kutoka inchi hii nzuri aliyowapa babu zao, na kuwatawanya mbali, ngambo ya muto Furati, kwa sababu wamemukasirikisha Yawe kwa kujitengenezea sanamu za Ashera.


“Atukuzwe Yawe ambaye amewapatia watu wake Waisraeli amani, kulingana na ahadi yake. Ametimiza ahadi zake zote njema alizozitoa kupitia kwa mutumishi wake Musa.


Kwa sababu hiyo laana inaiteketeza dunia, wakaaji wake wanateseka kwa ajili ya makosa yao. Wakaaji wa dunia wamepunguka, ni watu wachache tu waliobaki.


Angalia, Wakaldea wamechimba mifereji kuuzunguka muji; wanauzunguka kusudi wapate kuuteka; wanaushambulia. Vita, njaa na magonjwa vitaufanya muji utekwe na watu hao. Kweli mambo uliyotabiri yametokea. Unaona mwenyewe.


Yawe anasema hivi: Kama nilivyowaletea hasara watu hawa, ndivyo nitakavyowaletea mema niliyowaahidi.


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninawaletea Wayuda na wakaaji wote wa Yerusalema hasara zote nilizosema juu yao, kwa sababu mimi nilisema nao, lakini hawakunisikiliza; niliwaita, lakini hawakuniitikia.


Kama mukifuata masharti yangu na kushika amri zangu,


Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.


Waisraeli walitenda tena uovu mbele ya Yawe, naye akawaacha watawaliwe na Wafilistini kwa miaka makumi ine.


Waisraeli walitenda tena uovu mbele ya Yawe. Yawe akamutia nguvu mufalme wa Moabu aliyeitwa Mwana-Ngombe kusudi awashambulie Waisraeli, kwa sababu walitenda uovu mbele ya Yawe.


Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya mufalme wa Mesopotamia, jina lake Kusani, Yule-Mwovu-Sana. Wakamutumikia kwa muda wa miaka minane.


Waisraeli walitenda uovu mbele ya Yawe; naye akawatia katika mikono ya Wamidiani kwa muda wa miaka saba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ