“Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla
Kama mukitii amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa leo, mukimupenda Yawe, Mungu wenu, na kufuata njia zake na kushika amri, masharti na maagizo yake, basi, mutaishi na kuongezeka; naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika inchi ambayo munakwenda kuirizi.
Mumupende Yawe, Mungu wenu. Muitii sauti yake na kuambatana naye. Kama munafanya hivyo, mutapata maisha marefu na kuishi katika inchi ambayo Yawe aliwaahidi wazee wenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwamba atawapa.”
“Kwa hiyo mukuwe waangalifu kusudi musisahau kwamba Yawe aliposema nanyi kule kwenye milima ya Horebu katikati ya moto hamukumwona kwa umbo. Kwa sababu hiyo mufanye angalisho sana,
“Lakini mukuwe waangalifu na kufanya angalisho sana kusudi musisahau mambo yale muliyoona kwa macho yenu wenyewe, kusudi isitokee hata mara moja katika maisha yenu mambo hayo kusahaulika ndani ya mioyo yenu. Muwaelezee watoto wenu na wajukuu wenu
Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.
Mukuwe waangalifu kutii amri na sheria ambazo Musa, mutumishi wa Yawe, aliwaamuru: mumupende Yawe, Mungu wenu, mufuate anachotaka na kushika amri zake, mukae pamoja naye na kumutumikia kwa moyo wote na roho yote.”