Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 23:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nyuma ya muda murefu, Yawe aliwajalia Waisraeli amani kwa kuwaokoa na waadui zao pande zote. Wakati ule Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 23:1
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha kuishi maisha marefu na ya fanaka, akakufa na kukutana na wazee wake.


Wakati mufalme Daudi alipokuwa muzee sana, watumishi wake walimufunika kwa mablanketi, lakini, hata hivyo, hakuweza kupata joto.


Daudi akasema: “Yawe, Mungu wa Israeli, amewapa watu wake amani, naye ataishi Yerusalema kwa milele.


Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli waliokuwa viongozi wa jamaa, na majemadari wa maelfu na mamia na wakubwa wao waliomutumikia mufalme Daudi juu ya zamu za kuingia na kutoka. Kila mwezi katika mwaka, kundi tofauti la watu elfu makumi mbili na ine walishika zamu ya kufanya kazi.


Asa akatenda mambo yanayokuwa mazuri na sawa mbele ya Yawe, Mungu wake.


Alijenga miji yenye kuta za kuiimarisha inchi ya Yuda wakati ule wa amani, na kwa muda wa miaka ile, hapakutokea vita kwa maana Yawe alimupa amani.


Basi, Yosafati akatawala kwa amani, na Mungu akamupa amani pande zote.


Mukuje muone matendo ya Yawe. Muone maajabu aliyofanya katika dunia.


Kama vile ngombe wanavyopelekwa kwa kulishwa katika bonde, ndivyo Roho wa Mungu alivyowapumzisha watu wake. Ndivyo, ee Mungu ulivyowaongoza watu wako, nawe ukajipatia jina tukufu.


akawaambia: “Mimi sasa nina umri wa miaka mia moja na makumi mbili, na sina nguvu ya kufanya kazi zaidi. Tena Yawe ameniambia kwamba sitavuka muto Yordani.


Basi, Yoshua akaitwaa inchi yote kulingana na yote yale Yawe aliyomwambia Musa. Yoshua akaipatia Waisraeli ikuwe mali yao, wagawanyane kulingana na makabila yao. Kisha inchi nzima ikatulia, ikakuwa haina vita tena.


Wakati huu, Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi. Basi, Yawe akamwambia: “Wewe sasa umekuwa muzee wa miaka mingi, na kumebaki bado sehemu kubwa za inchi ambazo hazijatwaliwa.


Yawe akawapa amani kila pahali katika inchi kama vile alivyowaapia wazee wao. Hakuna adui yeyote aliyesubutu kuwashambulia maana Yawe alikuwa amewatia waadui hao katika mikono yao.


Sasa Yawe, Mungu wenu, amewapa wandugu zenu amani, kama vile alivyoahidi, basi, murudie kwenu katika inchi ambayo mulipewa na Musa mutumishi wa Yawe, ikuwe mali yenu, ni kusema ngambo ya muto Yordani.


Sasa, munakuwa na mufalme wa kuwaongoza. Kwa upande wangu, mimi ni muzee mwenye imvi, na wana wangu wako pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu nilipokuwa kijana mpaka sasa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ