Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 22:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Basi, watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakaachana na watu wa makabila mengine ya Israeli kule Shilo katika inchi ya Kanana, wakarudi kwao katika inchi ya Gileadi, inchi yao wenyewe walioirizi kwa amri ya Yawe kama vile alivyomwagiza Musa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 22:9
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kule, Abeneri akamusimika Isiboseti kuwa mufalme wa inchi ya Gileadi, Asheri, Yezereheli, Efuraimu na Benjamina na Israeli yote.


Vilevile, kwa maana makundi yao ya nyama iliongezeka kwa wingi sana, walisambaa upande wa mashariki mpaka kwenye viingilio vya jangwa lililoenea mpaka kwenye muto Furati.


Uwaponyeshe hao watu unaowapenda! Utuokoe kwa mukono wako! Utusikilize!


Makabila ya Rubeni na Gadi yalikuwa na mifugo mingi sana. Basi, walipoona kwamba eneo la Yazeri na Gileadi lilifaa kwa mifugo,


Musa akawaambia: Kama kweli mutafanya kama vile mulivyosema, basi hapahapa mbele ya Yawe, mutwae silaha zenu kwenda kwa vita.


na kurizi inchi. Mukisha kufanya hayo, mutarudi, maana mutakuwa bila kosa mbele ya Yawe na wandugu zenu Waisraeli. Kisha Yawe atakubali inchi hii ya upande wa mashariki wa Yordani kuwa mali yenu.


Wake zetu, watoto wetu na kondoo na ngombe, watabaki hapa katika miji ya Gileadi.


Ikiwa watu wa Gadi na wa Rubeni watavuka muto Yordani pamoja nanyi wakiwa na silaha zao chini ya uongozi wa Yawe, mukishinda na kuitwaa inchi hiyo, basi mutawapa inchi ya Gileadi ikuwe mali yao.


“Wakati ule niliwapa maagizo haya: ‘Yawe, Mungu wenu amewapa inchi hii upande wa mashariki wa muto Yordani ikuwe mali yenu. Sasa ninyi mashujaa kati ya wandugu zenu, mutwae silaha muvuke muto Yordani mukiwa mbele ya wandugu zenu Waisraeli.


Muwasaidie wandugu zenu Waisraeli mpaka Yawe atakapowajalia watulie pahali pao kama vile nanyi mulivyotulia, ni kusema nao vilevile warizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapatia huko ngambo ya Yordani. Nyuma ya hayo, mutaweza kurudia katika inchi yenu hii ambayo nimewapa ikuwe yenu!’


Basi, Musa akaondoka kwenye bonde la Moabu, akaenda kwenye mulima Nebo, akapanda juu ya kilele cha Pisiga kinachoelekeana na Yeriko. Hapo Yawe akamwonyesha inchi yote: toka Gileadi mpaka Dani,


pamoja na inchi za Gileadi, eneo la Wagesuri na Wamakati mulima wa Hermoni na inchi yote ya Basani mpaka Saleka;


ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya inchi ya Waamoni mpaka Aroeri kwa upande wa mashariki wa Raba.


nusu ya Gileadi, Astaroti, Edirei, ambayo ilikuwa ya mufalme Ogi wa Basani. Nusu ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, eneo hili walipewa kulingana na ukoo zao.


Walipofika kwenye muto Yordani wakiwa bado katika inchi ya Kanana, wakajenga mazabahu kubwa sana karibu na muto huo.


Watu wote wa Israeli, kutokea Dani mpaka Beri-Seba, pamoja na watu wa inchi ya Gileadi, wakakusanyika kule Misipa, mbele ya Yawe.


Kabila la Gileadi lilibaki ngambo ya Yordani. Kabila la Dani, kwa nini mulibaki ndani ya mashua? Kabila la Aseri lilitulia kule pembeni ya bahari, lilikaa katika kivuko chake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ