Yoshua 22:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
33 Habari hiyo ikawafurahisha Waisraeli, wakamushukuru Yawe na kuacha mipango yao ya vita na kusudi lao la kuharibu kabisa inchi iliyokuwa ya makabila ya Rubeni na Gadi.
Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.
Basi mukutano wote ukabaki kimya ukisikiliza maelezo ya Barnaba na Paulo juu ya vitambulisho na maajabu yote Mungu aliyofanya kwa njia yao katikati ya watu wa mataifa mengine.
Nasi hatukufarijiwa kwa kuja kwake tu, lakini vilevile kwa namna ile mulivyomufariji. Tito ametuelezea jinsi munavyokuwa na hamu kubwa ya kuniona, jinsi munavyohuzunika na jinsi munavyojitoa kwa ajili yangu. Kwa hivi sasa ninafurahi zaidi.
Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.
Kuhani Finehasi na wakubwa wa jamaa za Waisraeli waliokuwa pamoja naye waliposikia maneno hayo ya watu wa makabila ya Rubeni na Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakafurahi.
Basi, Finehasi mwana wa kuhani Eleazari pamoja na viongozi wenzake wakawaaga watu wa makabila ya Rubeni na Gadi wakaondoka katika inchi ya Gileadi, wakarudi Kanana kwa Waisraeli na kuwapa habari hizo.