Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 22:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Sisi hatukuwa na nia ya kumwasi sasa Yawe hata kidogo na kumwacha kwa kujenga mazabahu ya kutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto au sadaka za unga au sadaka zingine. Hatupendi kutolea sadaka pahali pengine isipokuwa juu ya mazabahu ya Yawe, Mungu wetu, inayokuwa katika makao yake.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 22:29
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yosefu akasema: “Hapana! Mimi siwezi kufanya hivyo! Yule tu aliyepatikana na kikombe changu ndiye atakayekuwa mutumwa wangu. Ninyi wengine wote murudi kwa amani kwa baba yenu.”


Lakini wao wakamwuliza: “Bwana, una maana gani kutuambia maneno kama hayo? Sisi watumishi wako hatuwezi kufanya jambo kama hilo!


Lakini, Naboti akamujibu: “Jambo la kukupa wewe urizi nilioupata kwa wazee wangu, Yawe alipitishe mbali.”


Lakini hata kama mukiniambia: ‘Tunamutegemea Yawe, Mungu wetu’, si huyohuyo ambaye Hezekia aliziharibu nafasi zake zote za kuabudu kwenye vilima pamoja na mazabahu zake na kuwaambia watu wa Yuda na Yerusalema: Munapaswa kuabudu mbele ya mazabahu hii ya Yerusalema tu?


Si ni huyu Hezekia ndiye aliyeharibu pahali pake pa kuabudia na mazabahu zake na kuwaamuru watu wote wa inchi ya Yuda na Yerusalema akisema: ‘Mutaabudu mbele ya mazabahu moja, na juu yake mutateketeza sadaka zenu?’


Hapana hata kidogo! Ingekuwa vile, namna gani basi Mungu angeweza kuhukumu dunia?


Hapana hata kidogo! Sisi tuliokufa kwa ajili ya zambi, namna gani tutaweza tena kuishi katika zambi?


Basi tuseme nini? Mungu hafuati haki? Hapana hata kidogo!


basi huko pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kusudi jina lake likae pale, hapo mutapeleka yote ninayowaamuru: sadaka zenu za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, na sadaka za kutimiza kiapo.


Kama tumemwacha Yawe tukajenga mazabahu yetu wenyewe kusudi tutoe sadaka za kuteketezwa kwa moto, za unga au za amani, basi Yawe atulipize kisasi.


Ndiyo maana tuliamua kujenga mazabahu hii, lakini si kwa ajili ya kutolea juu yake sadaka za kuteketezwa kwa moto wala sadaka zingine,


Tena tulifikiri kwamba ikiwa jambo kama hilo litasemwa juu yetu au juu ya wazao wetu katika siku zinazokuja, tutasema: ‘Muangalie mufano wa mazabahu ya Yawe ambayo wazee wetu waliijenga; sio kwa ajili ya kutolea juu yake sadaka za kuteketezwa kwa moto au sadaka zingine lakini kama ushuhuda kati yetu na ninyi’.


Kuhani Finehasi na wakubwa wa jamaa za Waisraeli waliokuwa pamoja naye waliposikia maneno hayo ya watu wa makabila ya Rubeni na Gadi na nusu ya kabila la Manase, wakafurahi.


Halafu watu wakamujibu: “Hatutaweza hata kidogo kumwacha Yawe na kuitumikia miungu mingine.


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ