Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 22:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Tena tulifikiri kwamba ikiwa jambo kama hilo litasemwa juu yetu au juu ya wazao wetu katika siku zinazokuja, tutasema: ‘Muangalie mufano wa mazabahu ya Yawe ambayo wazee wetu waliijenga; sio kwa ajili ya kutolea juu yake sadaka za kuteketezwa kwa moto au sadaka zingine lakini kama ushuhuda kati yetu na ninyi’.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 22:28
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Ahazi alipokwenda Damasiki kukutana na mufalme Tigilati-Pileseri, aliona mazabahu kule. Basi, akamutumia kuhani Uria mufano kamili na muchoro wa mazabahu hiyo.


Hakikisha kwamba umevitengeneza kwa mufano ulioonyeshwa kule juu ya mulima.


Siku hiyo, kutakuwa mazabahu kwa ajili ya Yawe katikati ya inchi ya Misri, na nguzo iliyotakaswa kwa ajili ya Mungu kwenye mpaka wa Misri.


Kazi wale makuhani wanayofanya ni mufano na kitambulisho kinachoonyesha jinsi mambo kamili yanavyopitika mbinguni. Maneno hayo yanalingana na yale yaliyomutokea Musa. Wakati Musa alipokuwa karibu ya kujenga Hema, Mungu alimwambia: “Ufanye angalisho kusudi upate kutengeneza kila kitu kufuatana na mufano niliokuonyesha kwa mulima.”


lakini tulitaka mazabahu hii ikuwe ushuhuda kati yetu na ninyi na vizazi vyetu vinavyokuja kwamba sisi tuna haki ya kumutumikia Yawe kwa sadaka zetu za kuteketezwa kwa moto na sadaka zetu zingine, na kwa sadaka zetu za amani, kusudi watoto wenu wasipate kuwaambia watoto wetu kwamba hawana fungu lolote lao kwa Yawe.


Sisi hatukuwa na nia ya kumwasi sasa Yawe hata kidogo na kumwacha kwa kujenga mazabahu ya kutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto au sadaka za unga au sadaka zingine. Hatupendi kutolea sadaka pahali pengine isipokuwa juu ya mazabahu ya Yawe, Mungu wetu, inayokuwa katika makao yake.”


Halafu akawaambia watu wote: “Jiwe hili ndilo litakalokuwa ushuhuda kwetu, maana limesikia maneno yote ambayo Yawe ametuambia. Kwa hiyo, litashuhudia juu yenu, kusudi musipate kumwasi Mungu wenu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ