Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 22:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Hamwoni kwamba Yawe ameweka muto wa Yordani kuwa mupaka kati yenu na sisi? Ninyi makabila ya Rubeni na kabila la Gadi hamuna fungu lolote lenu kwa Yawe.’ Hivyo watoto wenu wangeweza kisha kusababisha watoto wetu waache kumwabudu Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 22:25
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


Lakini watu wote wa Israeli walipoona kwamba mufalme hakuwajali, walimwambia: “Hatuna ushirika wowote na Daudi! Hatuna sehemu yetu kutoka kwa huyo mwana wa Yese. Murudie kwenu, enyi watu wa Israeli! Uitunze nyumba yako mwenyewe, ee Daudi.” Hivyo, watu wa Israeli wakarudi kila mutu kwake.


Yawe ataitupilia Israeli kwa sababu ya zambi za Yeroboamu ambaye alitenda zambi na kuwasukuma watu wa Israeli vilevile watende zambi.”


Mambo haya yalifanyika kwa sababu Yeroboamu alimukasirikisha Yawe, Mungu wa Israeli, kwa zambi yake na kwa kuwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Nikawajibu: “Mungu wa mbinguni atatufanikisha katika kazi hii, nasi tunaokuwa watumishi wake tutaanza kujenga. Lakini ninyi hamuna sehemu au haki wala ukumbusho katika Yerusalema.”


Wewe, ee Yawe, ndiwe riziki yangu kubwa, majaliwa yangu yako katika mikono yako.


Wewe hauna sehemu wala haki yoyote katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mukamilifu mbele ya Mungu.


Lakini sivyo inavyokuwa. Tuliijenga kwa kuogopa kwamba labda katika siku zinazokuja watoto wenu watawaambia watoto wetu: ‘Ninyi muko na uhusiano gani na Yawe, Mungu wa Israeli?


Ndiyo maana tuliamua kujenga mazabahu hii, lakini si kwa ajili ya kutolea juu yake sadaka za kuteketezwa kwa moto wala sadaka zingine,


lakini tulitaka mazabahu hii ikuwe ushuhuda kati yetu na ninyi na vizazi vyetu vinavyokuja kwamba sisi tuna haki ya kumutumikia Yawe kwa sadaka zetu za kuteketezwa kwa moto na sadaka zetu zingine, na kwa sadaka zetu za amani, kusudi watoto wenu wasipate kuwaambia watoto wetu kwamba hawana fungu lolote lao kwa Yawe.


Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ