Mufalme Yoasi akasahau mema yote aliyotendewa na Yoyada, baba ya Zakaria, akamwua mwana wake. Alipokuwa karibu kufa, alisema: “Yawe uangalie mambo haya na kuyalipiza.”
Nikimwambia mutu mwovu kwamba hakika atakufa, nawe haumwonyi au kumwambia aache mwenendo wake mubaya apate kuyaokoa maisha yake, basi, mutu huyo mwovu atakufa kwa uovu wake; lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.
Lakini kama yule mulinzi akiona waadui wanakuja naye hapigi baragumu na watu wakikosa kuonywa juu ya hatari inayokuja, waadui wakikuja na kumwua mutu yeyote kati yao, huyo mutu aliyekufa, atakuwa amekufa kwa kosa lake. Lakini mimi nitamulaumu mulinzi kwa kifo cha mutu huyo.
Nikimwambia mutu mwovu hivi: Wewe mutu mwovu hakika utakufa; lakini wewe hausemi chochote kwa kumwonya aachane na mwenendo wake, yule mutu atakufa kwa kosa lake; lakini nitakulaumu wewe kwa kifo chake.
basi huko pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kusudi jina lake likae pale, hapo mutapeleka yote ninayowaamuru: sadaka zenu za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, na sadaka za kutimiza kiapo.
Lakini sivyo inavyokuwa. Tuliijenga kwa kuogopa kwamba labda katika siku zinazokuja watoto wenu watawaambia watoto wetu: ‘Ninyi muko na uhusiano gani na Yawe, Mungu wa Israeli?