2 akawaambia: “Ninyi mumefuata yale yote Musa, mutumishi wa Yawe, aliyowaamuru na mumetii maagizo niliyowaamuru.
Wala hamukuwaacha wandugu zenu kwa muda ule wote murefu mpaka leo, lakini mumefuata kwa uangalifu amri ya Yawe, Mungu wenu.