Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 22:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Kwa nini, basi, mumeacha kumufuata Yawe? Mukimwasi Yawe leo, kesho atakasirikia sana Waisraeli wote pamoja.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 22:18
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa mara nyingine, Yawe aliwakasirikia Waisraeli, akamusukuma Daudi kuwatendea vibaya, akamwambia awahesabu watu wa Israeli na watu wa Yuda.


Lakini wewe au watoto wako mukigeuka na kuacha kunifuata, musiposhika amri zangu na masharti niliyowapa, mukienda kutumikia miungu mingine na kuiabudu,


Nyuma ya Yawe kutenga Israeli kutoka ukoo wa Daudi walimuweka Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mufalme. Naye Yeroboamu aliwasukuma watu wa Israeli kumwacha Yawe na kutenda zambi kubwa sana.


Shetani akaenda kinyume cha Waisraeli, akamushawishi Daudi kuwahesabu watu.


Basi, Yawe akawaletea Waisraeli ugonjwa mukali, ambao ulisababisa vifo vya Waisraeli elfu makumi saba.


Mashauri mabaya ya kumwua Amazia yalifanywa Yerusalema tangu alipomwacha Yawe, kwa hiyo akakimbilia Lakisi. Lakini waadui wakatuma watu Lakisi wakamwua kule.


Kisha Yosia akaondoa sanamu zote za kuchukiza zilizokuwa katika eneo lote la watu wa Israeli, na kuwasukuma watu wote wa Israeli kumutumikia Yawe, Mungu wao. Katika maisha yake yote hawakumwacha Yawe, Mungu wa babu zao.


Kisha Musa akamwambia Haruni na wana wake, Eleazari na Itamari: Musivuruge nywele zenu wala musipasue nguo zenu kwa kuomboleza, kama sivyo mutakufa na kuwaletea Waisraeli wote pamoja kasirani ya Yawe. Lakini wandugu zenu, ni kusema jamii yote ya Israeli, wanaweza kuomboleza kwa sababu ya moto huo Yawe alioleta.


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Kama ninyi mukikataa kumufuata, yeye atawaachilia tena katika jangwa, nanyi mutasababisha watu hawa wote waangamie.


Mukifanya hivyo wao watawapotosha watoto wenu wasimufuate Yawe, na kuwafanya waabudu miungu mingine, nayo hasira ya Yawe itawaka juu yenu, halafu atawaangamiza mara moja.


Nao wakawaendea watu wa makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase kule Gileadi wakawaambia:


“Watu wote wa Yawe wanauliza hivi: ‘Ni udanganyifu gani huu mumemufanyia Mungu wa Israeli? Mbona mumemwasi Yawe kwa kujenga mazabahu hii?


Akana mwana wa Zera alipokosa uaminifu katika vitu vitakatifu, kasirani haikuangukia Waisraeli wote pamoja? Tena Akana hakukufa tu yeye peke yake kwa sababu ya uovu wake.’ ”


Lakini Waisraeli hawakukuwa waaminifu juu ya vile vitu vilivyotolewa viangamizwe maana Akana mwana wa Karmi, mujukuu wa Zabedi, wa ukoo wa Zera, wa kabila la Yuda, alitwaa vimoja kati ya vitu vilivyoamriwa viteketezwe. Kwa hiyo hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli.


Waisraeli wametenda zambi, maana wamelivunja agano langu nililowaamuru washike. Wametwaa vimoja kati ya vitu vilivyotolewa viangamizwe. Wameviiba na kudanganya, wakaviweka pamoja na vitu vyao.


Nilipoona vazi moja zuri kutoka Sinari kati ya vitu tulivyonyanganya, vikoroti mia mbili vya feza na furushi ya zahabu yenye uzito wa vikoroti makumi tano vya feza, nikavitamani na kuvitwaa; nikavificha katika udongo ndani ya hema langu; na feza iko chini ya vitu hivyo.”


Kama mukimutii Yawe na kumutumikia na kusikiliza sauti yake bila kuiasi amri yake, kama ninyi wenyewe pamoja na mufalme anayewatawala mukimufuata Yawe, Mungu wenu, basi mutafanikiwa.


Samweli akawajibu: “Musiogope. Ingawa mumefanya uovu huu, musiache kumufuata Yawe, lakini mumutumikie kwa moyo wenu wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ