Na sasa, Yawe ametimiza ahadi yake, maana nimekuwa mufalme pahali pa baba yangu Daudi, na kukiikalia kiti cha kifalme cha Israeli kama vile Yawe alivyoahidi. Tena nimejenga nyumba ya kumwabudia Yawe, Mungu wa Israeli.
“Atukuzwe Yawe ambaye amewapatia watu wake Waisraeli amani, kulingana na ahadi yake. Ametimiza ahadi zake zote njema alizozitoa kupitia kwa mutumishi wake Musa.
Ukamwona kuwa wa haki mbele yako; ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi. Na ahadi yako ukaitimiza; maana wewe ni mwaminifu.
Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.