Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 21:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 Yawe akawapa amani kila pahali katika inchi kama vile alivyowaapia wazee wao. Hakuna adui yeyote aliyesubutu kuwashambulia maana Yawe alikuwa amewatia waadui hao katika mikono yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 21:44
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Israeli wakawakimbia Wayuda naye Mungu akawatia katika mikono yao.


Mipaka ya inchi yenu itakuwa kutoka bahari Nyekundu mpaka bahari ya Mediteranea na kutoka jangwa mpaka muto Furati. Nitawatia wakaaji wa inchi ile katika mikono yenu, nanyi mutawafukuza wawaondokee.


Mungu akasema: Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe na nitakupa raha.


Kama vile ngombe wanavyopelekwa kwa kulishwa katika bonde, ndivyo Roho wa Mungu alivyowapumzisha watu wake. Ndivyo, ee Mungu ulivyowaongoza watu wako, nawe ukajipatia jina tukufu.


Kuanzia Aroeri, muji unaokuwa kwenye ukingo wa bonde la Arnoni, na ule muji mwingine unaokuwa ndani ya bonde hili mpaka inchi ya Gileadi, hakuna muji wowote ambao hatukuweza kuushinda. Yawe aliitia miji yote katika mikono yetu.


“Mukienda kupigana vita na adui, naye Yawe akiwapa ushindi, na kuteka vitu,


Kwa hiyo kungali mapumziko ambayo Mungu anawatayarishia watu wake.


“Mukumbuke lile jambo ambalo Musa, mutumishi wa Yawe, aliwaamuru akisema: ‘Yawe, Mungu wenu, atawapa pahali pa kupumzika, na atawapa inchi hii’.


Mutawasaidia mpaka Yawe atakapowapa wandugu zenu vilevile pahali pa kupumzika, kama vile alivyowapa ninyi, nao vilevile warizi inchi ambayo wanapewa na Yawe, Mungu wenu. Kisha mutarudi katika inchi ambayo ni mali yenu na kuirizi, inchi ambayo mulipewa na Musa, mutumishi wa Yawe, ngambo ya muto Yordani.”


Hakuna mutu atakayekushinda siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa. Siku zote nitakuwa nawe wala sitakuacha hata kidogo.


Vilevile aliiteketeza miji ile mingine yote kwa moto na kuwaua wafalme wao wote kama vile Musa, mutumishi wa Yawe, alivyomwamuru.


Basi, Yoshua akaitwaa inchi yote kulingana na yote yale Yawe aliyomwambia Musa. Yoshua akaipatia Waisraeli ikuwe mali yao, wagawanyane kulingana na makabila yao. Kisha inchi nzima ikatulia, ikakuwa haina vita tena.


Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.


Wakamwambia: “Hakika Yawe ameitia inchi yote katika mikono yetu. Tena wakaaji wa inchi hiyo wametetemeka kwa sababu yetu.”


Sasa Yawe, Mungu wenu, amewapa wandugu zenu amani, kama vile alivyoahidi, basi, murudie kwenu katika inchi ambayo mulipewa na Musa mutumishi wa Yawe, ikuwe mali yenu, ni kusema ngambo ya muto Yordani.


Basi, watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakaachana na watu wa makabila mengine ya Israeli kule Shilo katika inchi ya Kanana, wakarudi kwao katika inchi ya Gileadi, inchi yao wenyewe walioirizi kwa amri ya Yawe kama vile alivyomwagiza Musa.


Nyuma ya muda murefu, Yawe aliwajalia Waisraeli amani kwa kuwaokoa na waadui zao pande zote. Wakati ule Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ