41 Jumla ya miji yote ambayo Walawi walipewa katika maeneo ya Waisraeli ilikuwa makumi ine na nane pamoja na mbuga zao za malisho.
Ninalaani hasira yao kali sana na kasirani yao isiyokuwa na huruma. Nitawatawanya katika inchi ya Yakobo, nitawasambaza katika inchi ya Israeli.
Kedemoti pamoja na mashamba yake ya malisho na Mefati pamoja na mashamba yake ya malisho.
Na watafundisha wazao wa Yakobo maagizo yako; watafundisha watu wa Israeli sheria yako. Walawi watafukiza ubani mbele yako, sadaka nzima za kuteketezwa juu ya mazabahu yako.
Basi, kulingana na amri ya Yawe, Waisraeli walichagua kutoka katika maeneo ya inchi zao, miji na vijiji vya malisho, wakawapa Walawi ikuwe sehemu yao.
Miji yote waliyopewa wazao wa Merari, ni kusema watu wa ukoo wa Walawi zilizobaki, ilikuwa kumi na miwili.
Kila mumoja kati ya miji hii ulizungukwa na mbuga za malisho.