Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 21:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Walipokuwa kule Shilo katika inchi ya Kanana viongozi wa ukoo za Walawi wakawaendea kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa za makabila yote ya Waisraeli,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 21:1
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninalaani hasira yao kali sana na kasirani yao isiyokuwa na huruma. Nitawatawanya katika inchi ya Yakobo, nitawasambaza katika inchi ya Israeli.


Haya ndiyo majina ya wakubwa wa jamaa za Waisraeli. Wana wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli: Hanoki, Palu, Hesironi na Karmi. Hao walikuwa babu za jamaa za Rubeni.


Eleazari mwana wa Haruni, alimwoa mumoja wa wabinti za Putieli, naye akamuzalia Finehasi. Hawa ndio waliokuwa wakubwa wa jamaa za Lawi.


Yawe akasema na Musa katika mabonde ya Moabu, ngambo ya muto Yordani karibu na Yeriko, akamwambia:


Hesabu ya miji mutakayowapa Walawi katika urizi wa Waisraeli itategemea ukubwa wa kabila; kabila kubwa litatoa miji mingi na kabila dogo litatoa michache. Kila kabila litatoa miji yake kwa ajili ya Walawi kulingana na eneo litakalorizi.


Haya ndiyo maeneo ya inchi ambayo Waisraeli walipewa katika inchi ya Kanana. Kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, pamoja na wakubwa wa ukoo za makabila ya Waisraeli waliyowagawanyia Waisraeli.


Wabinti hao wakamwendea kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wengine wakawaambia: “Yawe alimwamuru Musa atugawanyie na sisi wote inchi kama vile wanaume wa kabila letu wanavyogawanyiwa.” Basi kufuatana na amri ya Yawe, Yoshua akawapatia sehemu yao kama alivyowapa wanaume wa kabila lao.


Basi, kuhani Eleazari na Yoshua mwana wa Nuni, pamoja na viongozi wa makabila ya Waisraeli waligawanya sehemu hizo kwa kura mbele ya Yawe kwenye mulango wa hema ya kusanyiko kule Shilo. Basi, wakakamilisha kuigawanya inchi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ