Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 20:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Hii ndiyo miji iliyotengwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na wageni walioishi kati yao, kusudi mutu yeyote atakayemwua mwenzake bila kukusudia akimbilie kule asipate kuuawa na mwenye ruhusa ya kulipiza kisasi cha damu, mpaka pale atakapohukumiwa mbele ya mukutano wa watu wote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 20:9
5 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutajitengea miji sita kwa ajili ya makimbilio.


Miji hii itakuwa ya makimbilio kwa ajili ya Waisraeli na wageni wa kudumu au wa muda wanaokaa pamoja nao. Mutu yeyote akimwua mwingine bila kukusudia anaweza kukimbilia huko.


Mwuaji atakimbilia katika muji mumoja wa miji ile na kusimama kwenye mulango wa muji na kuwaelezea wazee wa muji ule maneno yake. Wazee watamupokea ndani na kumupa pahali pa kuishi pamoja nao.


Mwuaji ataendelea kuishi mule mpaka pale atakapohukumiwa mbele ya mukutano wote wa Waisraeli na vilevile mpaka pale yule Kuhani Mukubwa ambaye alikuwa na madaraka wakati ule atakapokufa. Nyuma ya pale mutu huyo ataweza kurudi katika nyumba yake katika muji ule pahali alipotoka wakati alipotoroka.”


Na ngambo ya muto Yordani, upande wa mashariki wa muji wa Yeriko, walichagua muji wa Bezeri unaokuwa kwenye jangwa katika mabonde ya eneo la kabila la Rubeni. Vilevile wakachagua Ramoti, kule Gileadi ambao ni muji wa kabila la Gadi na Golani kule Basani katika eneo la kabila la Manase.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ