Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 20:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Na ngambo ya muto Yordani, upande wa mashariki wa muji wa Yeriko, walichagua muji wa Bezeri unaokuwa kwenye jangwa katika mabonde ya eneo la kabila la Rubeni. Vilevile wakachagua Ramoti, kule Gileadi ambao ni muji wa kabila la Gadi na Golani kule Basani katika eneo la kabila la Manase.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 20:8
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Ahabu akakusanya manabii yapata mia ine, akawauliza: “Niende au nisiende kushambulia Ramoti-Gileadi?” Nao wakamujibu: “Kwenda! Yawe atakupatia ushindi.”


Mufalme Ahazia akaenda na Yoramu mwana wa Ahabu kupigana vita na Hazaeli mufalme wa Aramu kule Ramoti-Gileadi pahali Waaramu walipomwumizia Yoramu.


Tukateka miji yote katika sehemu za mabonde, za mwinuko, na vilevile eneo lote la Gileadi na Basani mpaka Saleka na Edirei, miji ya mufalme Ogi huko Basani.”


Alitenga muji wa Beseri katika bonde la jangwa kwa ajili ya kabila la Rubeni, muji wa Ramoti katika inchi ya Gileadi kwa ajili ya kabila la Gadi, na muji wa Golani katika inchi ya Basani kwa ajili ya kabila la Manase.


Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.


Hii ndiyo miji iliyotengwa kwa ajili ya watu wote wa Israeli na wageni walioishi kati yao, kusudi mutu yeyote atakayemwua mwenzake bila kukusudia akimbilie kule asipate kuuawa na mwenye ruhusa ya kulipiza kisasi cha damu, mpaka pale atakapohukumiwa mbele ya mukutano wa watu wote.


Watu wa uzao wa Lawi wa ukoo wa Gersoni, walipewa miji miwili katika nusu ya eneo la kabila la Manase: Golani, kule Basani, muji wa kukimbilia usalama, pamoja na mbuga zake za malisho, na Be-Estera pamoja na malisho yake.


Katika eneo la kabila la Rubeni walipewa Bezeri pamoja na mbuga zake za malisho, Yahazi pamoja na mbuga zake za malisho,


Katika eneo la kabila la Gadi walipewa Ramoti wa Gileadi, muji wa kukimbilia usalama, pamoja na mbuga zake za malisho, Mahanaimu pamoja na mbuga zake za malisho,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ