Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.
Hauna habari kwamba Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Yawe, mimi niliwatwaa manabii mia moja nikawaficha makumi tano tano katika pango, nikakuwa ninawapatia chakula na maji?
na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.
Lakini Yoseba binti ya mufalme Yoramu, dada ya Ahazia, alimutwaa kwa siri Yoasi mwana wa Ahazia, kutoka kati ya wana wa mufalme waliokuwa karibu kuuawa. Alimuficha yeye pamoja na mulezi wake katika chumba cha kulala. Hivyo walimuficha kusudi Atalia asimwone na kumwua.
Mufalme alimwamuru mwana wake Yerameli, Seraya mwana wa Azirieli na Selemia mwana wa Abudieli, wamukamate katibu Baruku na nabii Yeremia. Lakini Yawe aliwaficha.
Kwa njia ya imani wazazi wa Musa walimuficha kwa muda wa miezi mitatu nyuma ya kuzaliwa kwake. Kwa sababu waliona kwamba alikuwa mutoto mwenye sura nzuri, wala hawakuogopa amri ya mufalme.
Ilikuwa hivi vilevile kwa yule kahaba Rahaba. Mungu alimuhesabia haki kwa njia ya matendo yake, wakati alipowakaribisha wapelelezi na kuwatorosha kwa njia nyingine.
Basi, wale watu waliotumwa na mufalme wakawafuatilia kwa kupitia njia iliyokuwa imeelekea kwenye vivuko vya Yordani. Na mara tu walipoondoka katika muji, mulango wa muji ukafungwa.
Lakini yule kahaba Rahabu pamoja na watu wote wa nyumba ya baba yake, Yoshua akayaokoa maisha yao. Rahabu akaishi kati ya Waisraeli mpaka leo, kwa sababu aliwaficha wajumbe ambao Yoshua aliwatuma kwenda kuupeleleza muji wa Yeriko.