Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mufalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akisema: “Uwatoshe inje watu waliokuja katika nyumba yako maana wamekuja kuipeleleza inchi yote.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 2:3
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha miezi mitatu, Yuda akapata habari hii: “Tamari, muke wa mwana wako amekuwa kahaba, tena amepata mimba kwa kufanya ukahaba.” Basi, Yuda akaamuru: “Mumutoshe inje achomwe kwa moto!”


Lakini sisi tukamwelezea kwamba sisi ni watu waaminifu na wala si wapelelezi.


wakubwa wa Waamori walimwambia bwana wao, Hanuni: “Unazani kwamba Daudi kwa kukutumia watu wa kukufariji anamuheshimu baba yako? Daudi hakuwatuma watu hawa kwako kwa kuuchunguza na kuupeleleza muji halafu wauteke?”


Watumishi wa Abusaloma walipofika kwa yule mwanamuke, wakamwambia: “Ahimasi na Yonatani wako wapi?” Yule mwanamuke akawaambia: “Wamekwenda ngambo ya kijito.” Walipowatafuta na kuwakosa, wakarudi Yerusalema.


Lakini viongozi wa Waamoni wakamwambia mufalme: “Unazani ni kwa sababu ya heshima ya baba yako ndiyo maana Daudi anatuma wajumbe hawa wakuje kukufariji? Watu hawa ni wapelelezi waliotumwa kuja kuichunguza inchi kwa kuiangamiza na kuipeleleza.”


Mwovu anaponyeshwa siku ya hasara, anaokolewa siku ya kasirani!


Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe.


Pilato akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Angalia, nitawaletea naye hapa inje kusudi mupate kujua kwamba mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu.”


Alipokwisha kumukamata Petro, na kumutia katika kifungo, akamuweka chini ya ulinzi wa vikundi vine vya waaskari waliogomboana wane kwa wane. Naye alikusudia kumusambisha mbele ya watu nyuma ya sikukuu ya Pasaka.


Usiku, mbele ya kutimia kwa siku Herode aliyotaka kumusambisha mbele ya watu, Petro alikuwa amelala ndani ya chumba katikati ya waaskari wawili. Alikuwa amefungwa na minyororo miwili, nao walinzi walikuwa wakichunga mulango wa kifungo.


Wakafanya hivyo, wakamuletea Yoshua wale wafalme watano: mufalme wa Yerusalema, mufalme wa Hebroni, mufalme wa Yarmuti, mufalme wa Lakisi na mufalme wa Eguloni.


Mufalme wa muji wa Yeriko akaambiwa: “Wanaume wawili Waisraeli wameingia katika muji leo usiku kwa kuipeleleza inchi.”


Lakini, yule mwanamuke alikuwa amekwisha kuwaficha watu hao wawili. Basi, akawaambia wajumbe hao: “Ni kweli kwamba hao watu walikuja kwangu, lakini mimi sikujua wametoka wapi.


Sisera akamwambia: “Simama kwenye mulango wa hema. Mutu yeyote akikuja kukuuliza kama kuna mutu yeyote hapa, umwambie hakuna.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ