Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 2:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini mutu yeyote akitoka inje ya nyumba yako na kwenda katika njia atabeba lazima ya kifo chake yeye mwenyewe. Lakini kama mutu yeyote atakayekuwa ndani ya nyumba yako akiguswa tu, basi lazima ya kifo chake itakuwa juu yetu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 2:19
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akasema: “Ubebe wewe mwenyewe lazima ya kifo chako, maana umejishuhudia wewe mwenyewe kwa kinywa chako mwenyewe ukisema: ‘Nimemwua muchaguliwa wa Yawe.’ ”


Mutu mwovu anapomwua mutu wa haki akiwa katika kitanda ndani ya nyumba yake, basi si ni jambo la haki kwangu kumulipiza kwa sababu ya kumwanga damu kwa kumwondosha toka katika dunia?”


Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


Basi, ile damu itakuwa kitambulisho chenu cha kuonyesha nyumba mutakamokuwa. Nami nitakapoiona ile damu, nitawapita ninyi, hamutapatwa na hasara yoyote wakati nitakapoipiga inchi ya Misri.


Mutatwaa majani ya hisopo na kuyachovya katika damu ndani ya beseni na kupakaa vizingiti na miimo yote miwili ya milango ya nyumba zenu. Mutu yeyote asitoke inje ya nyumba usiku ule mpaka asubui.


Maana Yawe atapita kuwaua Wamisri. Lakini atakapoona damu iliyopakwa kwenye vizingiti na miimo ya nyumba zenu, atapita na wala hatamuruhusu mwangamizaji kuingia katika nyumba zenu na kuwaua.


Mwanaume akilala na mumoja wa wake za baba yake, anamupatisha baba yake haya, wote wawili wanapaswa kuuawa. Mwanaume huyo na mwanamuke huyo wote wawili watauawa na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.


Mutu yeyote anayemulaani baba yake au mama yake, anapaswa kuuawa. Amemulaani baba au mama yake, kwa hiyo damu yao itakuwa juu yake mwenyewe.


Atakayekutiwa juu ya paa la nyumba asishuke ndani yake kwa kutwaa kitu.


Lakini wakati Wayuda walipingana naye na kumutukana, kwa hiyo akakunguta mavumbi yaliyorukia juu ya nguo zake na kuwaambia: “Lazima ya kuazibiwa kwenu ikuwe juu ya kichwa chenu wenyewe! Mimi sina kosa. Tangu sasa nitawaendea watu wa mataifa mengine.”


Ndiyo maana ninahakikisha mbele yenu leo kwamba mimi sitabeba lazima ya damu ya hata mumoja wenu atakayepotea.


Lakini Paulo akamwambia yule mukubwa wa jeshi pamoja na waaskari wengine: “Watu hawa wasipobakia ndani ya chombo hamutaokolewa.”


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Kwa hiyo basi, tafazali muniapie kwa jina la Yawe kwamba mutanitendea mema mimi na jamaa yangu kama vile mimi nilivyowatendea mema, na munipe uhakikisho kamili.


Wale watu wakamujibu: “Uzima wenu ni uzima wetu! Kama hamutaifichua siri yetu, Yawe atakapotupa inchi hii, tutakutendea kwa wema na uaminifu.”


Lakini kama ukimwambia mutu yeyote juu ya shuguli hii yetu, basi, sisi hatutatimiza kiapo ulichotuomba tukuapie.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ