Yoshua 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Kwa hiyo basi, tafazali muniapie kwa jina la Yawe kwamba mutanitendea mema mimi na jamaa yangu kama vile mimi nilivyowatendea mema, na munipe uhakikisho kamili.
Kwa hiyo uniapie kwa jina la Mungu kwamba hautanidanganya mimi au watoto wangu au wazao wangu. Kadiri mimi nilivyokutendea mema, vivyo hivyo nawe unitendee mema mimi na inchi hii unamokaa.”
Lakini tafazali usinisahau wakati mambo yatakapokuendea wewe vizuri. Unitendee mema na kusema juu yangu mbele ya mufalme, nipate kutoka humu katika kifungo.
Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli.
Basi, ile damu itakuwa kitambulisho chenu cha kuonyesha nyumba mutakamokuwa. Nami nitakapoiona ile damu, nitawapita ninyi, hamutapatwa na hasara yoyote wakati nitakapoipiga inchi ya Misri.
Na kama watajifunza mwenendo wa watu wangu kwa moyo wote, wakiapa kwa jina langu, wakisema “Kama vile Yawe anavyoishi”, kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Bali, basi watastawi katikati ya watu wangu.
Tutakapokuja katika inchi hii, funga kamba hii nyekundu kwenye dirisha ambalo umetuteremushia. Uwakusanye hapa kwako baba yako, mama yako na kaka zako na jamaa yote ya baba yako.
Lakini mutu yeyote akitoka inje ya nyumba yako na kwenda katika njia atabeba lazima ya kifo chake yeye mwenyewe. Lakini kama mutu yeyote atakayekuwa ndani ya nyumba yako akiguswa tu, basi lazima ya kifo chake itakuwa juu yetu.
Yoshua akawaambia wale wapelelezi wawili walioipeleleza inchi hiyo: “Muende katika nyumba ya yule kahaba; mumulete yule mwanamuke na wale wote ambao ni wandugu zake kama mulivyomwapia.”
Daudi akamwuliza: “Utaweza kunipeleka kwenye kundi lile?” Kijana akamujibu: “Ikiwa utaniapia kwa jina la Mungu kwamba hautaniua, wala kunitia katika mikono ya bwana wangu, nitakupeleka.”