9 Kwa vile eneo lililopewa kabila la Yuda lilikuwa kubwa kuliko kabila hilo lilivyohitaji, sehemu ya eneo lake lilipewa kabila la Simeoni.
Ninalaani hasira yao kali sana na kasirani yao isiyokuwa na huruma. Nitawatawanya katika inchi ya Yakobo, nitawasambaza katika inchi ya Israeli.
Lakini wote walipopima kiasi walichookota katika kipimo cha litre ine, walitambua kwamba aliyeokota kingi hakukuwa na cha zaidi na aliyeokota kidogo, hakupungukiwa. Kila mumoja alikuwa ameokota kiasi alichoweza kula.
Eneo linalopakana na eneo la Rubeni kutoka mashariki mpaka magaribi litakuwa la kabila la Yuda.
Kabila kubwa litapewa sehemu yao kubwa na dogo litapewa sehemu yao ndogo. Kila kabila litapewa urizi wake kulingana na hesabu ya watu wake.
Kura ya tatu ilizipata ukoo za kabila la Zebuluni. Eneo lao lilienea mpaka Saridi.